Ajilo (pia: Agilus, Agile, Aile, Ayeul, El; Burgundy, leo nchini Ufaransa, 580 hivi – Rebais, Ufaransa wa leo, 650 hivi) alikuwa abati wa kwanza wa monasteri ya Rebais kuanzia mwaka 636 hadi kifo chake.

Alipoingia utawani huko Luxeuil akiwa bado mtoto, mwalimu wake alikuwa Kolumbani. Baada ya kupata upadirisho alifanya kwa mafanikio umisionari huko Bavaria pamoja na Eustasi wa Luxeuil[1].

Tangu kale anaheshimiwa na Kanisa Katoliki kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa hasa tarehe 30 Agosti[2].

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

Marejeo hariri

  Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.