Apiani wa Kaisarea

Apiani wa Kaisarea (Lycia, leo nchini Uturuki, 287 hivi - Kaisarea Baharini, leo nchini Israeli, 305 hivi) alikuwa kijana msomi ambaye aliongokea Ukristo.

Picha takatifu ya Mt. Apiani.

Kwa sababu ya imani yake, alijaribu kuzuia ibada ya Kipagani, ambayo Wakristo walilazimishwa kuishiriki katika dhuluma ya kaisari Masimino Daia: alimkaribia kishujaa gavana Urbano na kumshika mkono. Hapo akachomwa moto miguu na kutoswa na askari baharini [1].

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu mfiadini.

Sikukuu yake huadimishwa tarehe 2 Aprili[2].

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

Viungo vya nje hariri

  Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.