Arnulfi wa Soissons

Arnulfi wa Soissons (pia: Arnoul, Arnulf, Arnold; Tiegern, leo nchini Ubelgiji, 1040 - alifariki Oudenburg, Ubelgiji, 1087) alikuwa askari, halafu mmonaki Mbenedikto, mkaapweke, abati, na kuanzia mwaka 1080 askofu wa Soissons, leo nchini Ufaransa.

Mt. Arnulfi katika mavazi ya askofu.

Alipojitokeza mwingine kama askofu wa mji huo, aliona afadhali kurudi utawani badala ya kushindana naye. Hivyo akaanzisha monasteri alipofariki[1].

Papa Kalisti II alimtangaza kuwa mtakatifu tarehe 6 Januari 1120.

Sikukuu yake ni tarehe 14 Agosti[2].

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

Marejeo hariri

  • H. Claeys, Saint Arnold. Évêque de Soissons Apôtre de la Flandre. Fondateur de l`Abbaye d`Oudenbourg. 1889.
  • R.I.A. Nip (ed.), Lisiardus, Hariulfus. Vitae, Miracula, Translatio et alia Hagiographica sancti Arnulphi episcopi Suessionensis (= Corpus Christianorum. Continuatio Mediaevalis 285), Turnhout: Brepols Publishers, 2015 (ISBN 978-2-503-05301-1)

Viungo vya nje hariri

  Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.