Ayatollah (kwa Kiajemi: آيت الله; kwa Kiarabu: آية الله ayatu 'llah - "alama ya Allah/Mungu") ni cheo cha kiongozi wa kidini katika Uislamu wa Shia hasa nchini Uajemi na pia Iraq.

Cheo cha ayatollah hakilingani na kuhani au askofu katika dini nyingine. Kinafanana zaidi na profesa wa chuo kikuu kwa sababu ayatollah hutambuliwa baada ya kumaliza masomo yake na kufundisha kwa muda fulani. Akionekana anajua mambo yake na anaheshimiwa na akina ayatollah waliomtangulia, ataanza kuitwa hivyo.

Wachache huitwa "ayatollah mkubwa" wakikubaliwa na wafuasi wengi sana, pia na wenzao.

Ayatollah aliyejulikana sana duniani alikuwa Ruhollah Khomeini (17 Mei 1900 - 3 Juni 1989) aliyeanzisha mapinduzi ya Kiislamu nchini Uajemi na kuwa kiongozi wa jamhuri ya Kiislamu.

Mwingine ni Ayatollah Mkubwa Ali Al-Hoessein al-Sistani ambaye ni kiongozi mkuu wa Washia nchini Iraq.

Makala hii kuhusu mambo ya dini bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu mada hii kama historia yake au uenezi wake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.