Berardo (alizaliwa Carbio, Umbria, Italia, karne ya 12) akafia dini ya Ukristo kwa kuchomwa kwa upanga huko Marakesh, leo nchini Morocco pamoja na Ndugu Wadogo wenzake Petro wa San Gemini, Oto, mapadri kama yeye, Akursius na Adiutus, mabradha.

Berardo na wenzake.

Ndio Wafransisko wafiadini wa kwanza. Aliposikia habari zao, Fransisko wa Asizi alishangilia, "Sasa kweli naweza kusema nina Ndugu Wadogo watano". Ndiye aliyekuwa amewatuma kumhubiri Kristo kwa Waislamu, nao wakafanya hivyo kwanza Sevilia, Hispania, hadi walipofukuzwa kwenda Moroko.

Wote wanaheshimiwa na Kanisa Katoliki kama watakatifu, hasa tangu mwaka 1481 walipotangazwa na Papa Sixtus IV.

Sikukuu yao ni tarehe 16 Januari[1], siku ya kifodini chao mwaka 1220.

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

Viungo vya nje hariri