Capulana (pia huandikwa "kapulana", au kwa Changana "nguvu" au "vemba") ni aina ya vazi linalovaliwa zaidi nchini Msumbiji lakini pia katika maeneo mengine ya kusini-mashariki mwa Afrika. Ni vazi lenye urefu wa mita 2 kwa mita 1. Iinaweza kutumika kama sketi ya kukunja, mavazi au inaweza kutumiwa kwa kumbeba mtoto mgongoni. Inachukuliwa kuwa kipande kamili cha nguo.Capulana imekuwepo Msumbiji tangu kuanzishwa kwa njia za biashara za Waarabu na Wahindi. Zilipokelewa kutoka kwa wafanyabiashara wa Kihindi kama njia ya biashara ya bidhaa zingine. Kwanza, walikuja hasa katika rangi tatu: nyekundu, nyeupe, na nyeusi. Nyeupe iliwakilisha ulinzi wa mababu, nyeusi iliwakilisha uovu, na nyekundu iliwakilisha roho ya vita.Baada ya wakati huu, wananchi wa Msumbiji walipendelea kutumia capulanas kuliko ngozi za wanyama zilizotumiwa kitamaduni.

mwanamke wa Msumbiji katika vazi la capulana

Leo, kuna aina nyingi za capulanas za mitindo na rangi mbalimbali. Capulana mara nyingi huvaliwa na hijabu na blauzi iliyorekebishwa nchini Msumbiji. Hutumika kwa namna mbalimbali, ikiwa ni pamoja na mavazi ya kawaida ya kila siku, kubeba mizigo mizito, au hata iliyotengenezwa kwa ubunifu kwa sababu ya hafla maalum.Rangi na mitindo ya kitamaduni ya awali ya capulana inatamaniwa sana na inauzwa kwa bei ya juu katika masokoni leo. Nchini Msumbiji ina thamani kubwa na wanazingatiwa sana kuwa ni nzuri.

Rangi ya kunga'aa ya capulana mara nyingi hutolewa kama zawadi kwa wanawake. Wanandoa wengine hutengeneza mavazi yanayofanana ya capulana kwa hafla maalum au kwa sababu kuu kama vile ndoa ya kitamaduni kati ya hao wawili.two.[1]

Marejeo hariri

  1. "Capulanas". Iliwekwa mnamo 2013-12-17.