Chasi (au Kialagwa au Algwaisa) ni mojawapo ya lugha za Kikushi zinazotumika nchini Tanzania. Inazungumzwa na Wasi: kabila hili sehemu zote wanazokaa wenyewe huongea lugha hii na ndiyo asili yao ya wazazi wao waliowakuta. Lugha hii si ya Kibantu, kwani huendana na Kifiomi, Kiiraqw na Kiburunge.

Mwaka wa 2003 idadi ya wasemaji wa Kialagwa imehesabiwa kuwa watu 30,000. Kufuatana na uainishaji wa lugha kwa ndani zaidi Kialagwa iko katika kundi la Kikushi.

Viungo vya nje hariri

Marejeo hariri

  • Maho, Jouni & Bonny Sands. 2002. The languages of Tanzania: a bibliography. (Orientalia et africana gothoburgensia, no 17.) G”teborg: Acta Universitatis Gothoburgensis. Pp ix, 428. ISBN 91-7346-454-6

Kitabu hiki kinataja marejeo mengine kama:

  • Mous, Maarten. 2001. Basic Alagwa syntax. In: New data and new methods in Afroasiatic linguistics: Robert Hetzron in memoriam, uk.125-135. Kuhaririwa na Andrzej Zaborski. Wiesbaden: Otto Harrassowitz Verlag.
  Makala hii kuhusu mambo ya lugha bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Chasi kama historia yake, uenezi au maendeleo yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.