Elia wa Enna (pia: Elia Kijana; jina la kuzaliwa kwa Kiitalia: Giovanni Rachites; kwa Kigiriki: 'Ιωάννης Ραχίτης; Enna, Italia, 822/823 - Thesalonike, Ugiriki, 17 Agosti 903) alikuwa Mkristo wa Mashariki kutoka Sicilia, leo nchini Italia, aliyefanywa mtumwa na Waarabu walioteka kisiwa hicho akapelekwa Afrika. Kisha kuachiliwa, alifanya umisionari hadi alipolazimika kukimbia.

Picha takatifu ya kwake pamoja na Mt. Filarete wa Seminara.

Huko Yerusalemu akawa mmonaki sehemu mbalimbali hadi Uajemi na Afrika tena. Kisha kuteswa sana na Waislamu kwa ajili ya imani yake, alirudi kwao akaanzisha monasteri mbalimbali hadi Italia Kusini akishika kwa ushujaa maisha magumu na ya sala [1].

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 17 Agosti[2].

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

  1. https://www.santiebeati.it/dettaglio/46850
  2. Martyrologium Romanum

Marejeo hariri

  • Giuseppe Rossi Taibbi, Vita di Sant'Elia il Giovane, Istituto Siciliano di Studi Bizantini e Neoellenici, 1962
  • A. Basile, Il monastero di Sant'Elia nuovo e di San Filarete presso Seminara in ASCL XIV, 1945, n. 2;
  • N. Ferrante, Il monastero di S. Elianovo e Filareto di Seminara in Historica XXXII (1979);
  • Anonimo (monaco), Vita e Opere Del Nostro Santo Padre Elia Il Giovane (Siculo) (a cura editoriale e traduzione in Neogreco Monaco Aghiorita Cosma, traduzione in italiano Stefano dell'Isola), Giuseppe Pontari Editore, Roma
  Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.