Eva mpya (kwa Kilatini: Nuova Eva) ni jina linalotumiwa tangu karne ya 2 katika teolojia ya Mababu wa Kanisa, kama vile Yustino[1] na Irenei[2], kwa Bikira Maria kama mwenzi wa Adamu mpya, Yesu (1Kor 15:45).

"Dhambi ya asili" - Giovanni Stradano, 1583.

Tangu karne za kwanza za Kanisa, wanateolojia hao waliona nafasi ya pekee ya Maria katika mpango mzima wa wokovu wa binadamu ulioandaliwa na Mungu Baba, ulioahidiwa mara baada ya dhambi ya asili (Mwa 3:15) na uliotekelezwa katika utimilifu wa nyakati (Gal 4:4-5).

Kama vile Eva kwa uasi wake alivyochangia dhambi ya Adamu kwa hasara ya wazao wao wote, Maria kwa imani yake (Lk 1:45) alichangia kazi ya Mwanae kwanza kwa kumzaa (Mk 6:3), halafu kwa kumfuata hadi Kalivari aliposimama chini ya msalaba wa Yesu na kupokea kutoka kwake mwanafunzi wake mpendwa (Yoh 19:25-27)[3].

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

  1. Allert, Craig D. (2002). Revelation, Truth, Canon and Interpretation: Studies in Justin Martyr's Dialogue with Trypho. Brill. uk. 34. 
  2. Schaff, Philip. "Introductory Note to Irenæus Against Heresies", The Apostolic Fathers with Justin Martyr and Irenaeus, (Alexander Roberts and James Donaldson, eds.) 1885
  3. The Roman Breviary contains a Mass in which Mary is described, "Mary, the New Eve, is the First Disciple of the New Law.": http://www.ibreviary.com/m/preghiere.php?tipo=Preghiera&id=725 "Masses of the BVM: 20 Mary, the New Eve", iBreviary]

Marejeo hariri

  • Gambero, Luigi. Mary and the Fathers of the Church: The Blessed Virgin Mary in Patristic Thought, trans. Thomas Buffer (San Francisco: Ignatius Press, 1999).