Futi (kiing. foot) ni kipimo cha urefu wa 30.48 sentimita au inchi 12. Asili yake ni urefu wa sehemu ya kanyagio ya mguu wa mwanadamu. Si kipimo sanifu cha kimataifa bali ni kizio cha vipimo vya Uingereza.

Futi zenyewe = miguu hutofautiana ukubwa kati ya watu - hivyo futi ilikuwa kipimo tofauti kati ya nchi na nchi. Leo hii inatumiwa zaidi Marekani na katika nchi chache za Jumuiya ya Madola

Kifupi chake ni ft. au inaandikwa hivyo: futi 5 inchi 11 = 5' 11".

Neno "futi" latumiwa pia kutaja chenezo au rula (chombo cha kupima urefu wa kitu).

Kipimo cha futi kiliingia katika Kiswahili tangu ukoloni wa Uingereza. Kimechukua nafasi ya vipimo asilia vya Kiswahili kama shubiri (takriban 25 cm) na ziraa (takriban 50 cm).

Kihistoria urefu wa futi ilikuwa tofauti kati nchi na nchi. Leo hii inatumiwa zaidi Marekani lakini pia kwa uzoefu katika nchi zinazotumia sana lugha ya Kiingereza hata kama rasmi zimeshakubali vipimo sanifu vya kimataifa SI.