Hedwiga (kwa Kijerumani Hedwig; kwa Kipolandi Jadwiga, linatamkwa jadˈviɡa; Budapest, Hungaria, 1373/1374 - Krakov, Polandi, 17 Julai 1399) alikuwa malkia wa Polandi na Lituania.

Malkia Hedwiga leo anaheshimiwa kama mtakatifu.
Ngao yake.
Vazi maalumu la ibada la Jadwiga.

Kuanzia mwaka 1384 hadi kifo chake alitawala nchi ya Poland akiitwa 'mfalme' badala ya 'malkia', ili kusisitiza kwamba hakuwa tu mke wa mtawala halisi[1].

Alizaliwa katika ukoo wa Wakapeti wa Anjou, binti wa mwisho wa mfalme Luis I wa Hungaria na Elizabeti wa Bosnia.[2].

Kwa kuolewa na Ladislaus wa Lituania, alimfanya abatizwe akaeneza Ukristo katika nchi hiyo ya Kipagani [3].

Tangu zamani anaheshimiwa na Kanisa Katoliki kama mtakatifu na msimamizi wa kila malkia. Papa Yohane Paulo II ndiye aliyemtangaza rasmi mwenye heri tarehe 8 Agosti 1986 na mtakatifu tarehe 8 Juni 1997.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe aliyofariki dunia[4].

Picha hariri

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

  1. Hedvigis Rex Polonie: M. Barański, S. Ciara, M. Kunicki-Goldfinger, Poczet królów i książąt polskich, Warszawa 1997, also Teresa Dunin-Wąsowicz, Dwie Jadwigi (The Two Hedwigs) Archived 9 Februari 2012 at the Wayback Machine.
  2. Norman Davies (2005). Jadwiga (chapter Jogalia). God's Playground: A History of Poland in Two Volumes, Volume 1 94-96. Oxford University Press. Iliwekwa mnamo 10 Aprili 2012.
  3. https://www.santiebeati.it/dettaglio/92253
  4. Martyrologium Romanum
  5. Psałterz floriański. Jalada kutoka ya awali juu ya 2009-05-10. Iliwekwa mnamo 2011-11-16.

Marejeo hariri

Viungo vya nje hariri

 
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
  Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.