Herode Mkuu (73 KK hivi - 4 KK) ni jina la heshima linalotumika kumtajia mtu maarufu zaidi wa ukoo wa kifalme wa Yudea katika karne ya 1 KK, yaani Herode (kwa Kiebrania הוֹרְדוֹס, Hordos, kwa Kigiriki: Ἡρῴδης, Hērōdēs).[1][2][3][4][5]

Herode Mkuu.
Herode Mkuu.
Herode akiteka Yerusalemu.
Hekalu la Yerusalemu.
Mamajusi mbele ya Herode.
Mchoro wa Duccio di Buoninsegna kuhusu Mauaji ya watoto wachanga yaliyoagizwa na Herode.

Akiwa kwa asili mtu wa kabila la Waedomu upande wa baba na Myahudi upande wa mama, alitawala Yudea yote chini ya himaya ya Dola la Roma.

Mkatili hasa, aliua hata mke wake mmojawapo na watoto watatu.

Ingawa alifuata dini ya Uyahudi na kuanza kazi kubwa ya kupanua na kupamba hekalu la Yerusalemu, alizingatia zaidi ustaarabu wa Kigiriki na kuendeleza miji kipagani.

Ni maarufu zaidi kutokana na taarifa za Injili ya Mathayo kuhusu jinsi alivyopokea kutoka kwa Mamajusi habari ya kuzaliwa kwa Mfalme wa Wayahudi, Yesu. Kwa hofu yake aliposhindwa kumtambua mtoto huyo, aliagiza wauawe watoto wote wa kiume chini ya umri wa miaka 2.

Familia hariri

Familia ya Herode Mkuu
Mke Watoto
Doride
  • Antipatro, alifariki 4 KK
Mariamne I
  • Aleksanda, alifariki 7 KK
  • Aristobulo, alifariki 7 KK
  • Salampsio
  • Cypro
Mariamne II
  • Herode II, alifariki 6
  • Herode Filipo
Malthace
  • Arkelao, mfalme mdogo wa Yudea
  • Herode Antipa, mfalme mdogo wa Galilaya
  • Olimpia
Kleopatra wa Yerusalemu
  • Herode Filipo II, mfalme mdogo wa Perea
  • Herode
Pallade
  • Fasaele
Fedra
  • Rossane
Elpide
  • Salome

Tanbihi hariri

  1. Richardson, Peter. Herod: King of the Jews and friend of the Romans, (Continuum International Publishing Group, 1999) pp. xv–xx.
  2. Knoblet, Jerry. Herod the Great (University Press of America, 2005), p. 179.
  3. Rocca, Samuel. Herod's Judaea: a Mediterranean state in the classical world (Mohr Siebeck, 2008) p. 159.
  4. Millar, Fergus; Schürer, Emil; Vermes, Geza. The History of the Jewish People in the Age of Jesus Christ (Continuum International Publishing Group, 1973) p. 327.
  5. Wright, N. T. The New Testament and the People of God (SPCK, 1992), p. 172.

Marejeo hariri

  • Brandon, S. G. F. (1962). "Herod the Great: Judaea's Most Able but Most Hated King". History Today 12: 234–242. 
  • Grant, Michael (1971). Herod the Great. New York: American Heritage Press. ISBN 0-07-024073-6. 
  • Günther, Linda-Marie (hg.) Herodes und Jerusalem (Stuttgart: Franz Steiner Verlag, 2009).
  • Günther, Linda-Marie (hg.) Herodes und Rom (Stuttgart: Franz Steiner Verlag, 2007).
  • Jacobson, David M. and Nikos Kokkinos (eds). Herod and Augustus: Papers Held at the Institute of Jewish Studies Conference, University College London, 21–23 June 2005 (Leiden, Brill, 2009) (IJS Studies in Judaica, 6).
  • Knoblet, Jerry. Herod the Great. Lanham, Maryland: University Press of America, 2005.
  • Kokkinos, Nikos. The Herodian Dynasty: Origins, Role in Society and Eclipse (Sheffield: Sheffield Academic,1998).
  • Marshak, Adam Kolman (2006). "The Dated Coins of Herod the Great: Towards a New Chronology". Journal for the Study of Judaism 37 (2): 212–240. doi:10.1163/157006306776564700. 
  • Netzer, Ehud. The Architecture of Herod, the Great Builder (Tübingen: Mohr Siebeck, 2006).
  • Perowne, Stewart (1956). The Life and Times of Herod the Great. New York: Abingdon Press. 
  • Richardson, Peter. Herod the King of the Jews and Friend of the Romans (Edinburgh: 1999).
  • Roller, Duane W. (1998). The Building Program of Herod the Great. Berkeley: University of California Press. ISBN 978-0-520-91935-8. 
  • Sandmel, Samuel (1967). Herod: Profile of a Tyrant. Philadelphia: Lippincott. 
  • Schwentzel, Christian-Georges (2011). Hérode le Grand. Paris: Pygmalion.
  • Witztum, Eliezer. King Herod: A Persecuted Persecutor. A Case Study in Psychohistory and Psychobiography (Berlin and New York, Walter de Gruyter, 2006).
  • Zeitlin, Solomon (1963). "Herod: A Malevolent Maniac". Jewish Quarterly Review 54: 1–27. doi:10.2307/1453457. 
  • Zeitlin, Solomon (1962–1978). The Rise and Fall of the Judean State. Philadelphia: The Jewish Publication Society. 

Viungo vya nje hariri

  Makala hii kuhusu mtu wa Biblia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Herode Mkuu kama habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.