Hifadhi ya Taifa ya Mosi-oa-Tunya

Hifadhi ya Taifa ya Mosi-oa-Tunya, ni hifadhi ya Urithi wa Dunia wa UNESCO [1] ambapo hupatikana nusu ya mto Mosi-oa-Tunya unaojulikana duniani kote kama Maporomoko ya maji ya Victoria kwenye Mto Zambezi . Mto huu unatengeneza mpaka kati ya Zambia na Zimbabwe, kwa hivyo maporomoko hayo yanashirikiwa na nchi hizo mbili, na mbuga hiyo ni 'pacha' na Mbuga ya taifa ya Victoria Falls upande wa Zimbabwe. [2]

Mtazamo wa angani wa mbuga hiyo yenye kundi la nyati.

'Mosi-oa-Tunya' imenatokana na lugha ya Kololo au Lozi na jina hilo sasa linatumika kote Zambia, na katika sehemu za Zimbabwe. [2]

Marejeo hariri

  1. Unesco World Heritage List website accessed 1 March 2007
  2. 2.0 2.1 Camerapix: "Spectrum Guide to Zambia." Camerapix International Publishing, Nairobi, 1996.