Historia ya Fiji inahusu nchi hiyo ya visiwani katika bahari ya Pasifiki.

Historia ya awali hariri

Wakazi wa visiwa vya Fiji, wanaaminika kuwa walitokana na wavuvi wa masafa marefu ambao walifika katika visiwa hivyo zaidi ya miaka 3500 iliyopita.

Shughuli za ufinyanzi katika jamii ya watu wa kabila la Walapita zimeonekana kutawala maeneo mengi sana katika visiwa vya Fiji, nazo ni ushahidi wa kuwa Fiji imekuwa ikikaliwa na watu tangu miaka 3500 hadi 1000 kabla ya Kristo.

Japokuwa jamii ya kabila hilo ndio wanaoaminika kuwa wa kwanza kuishi katika visiwa vya Fiji, lakini hali hii inatiliwa shaka kutokana na jamii ya kabila la Wamelanesia kuwepo kwa wingi sana katika visiwa hivyo, hali inayoashiria kuwa pengine kabila hilo pia limekuwepo tangu kale.

Utamaduni katika visiwa vya Fiji umekuwa ukifanana sana na ule wa jamii ya Wamelanesia ambao hupatikana magharibi mwa bahari ya Pasifiki, lakini utamaduni huo umekuwa ukifananishwa sana na ule wa jamii za Samoa na Tonga.

Shughuli za biashara katika mataifa hayo matatu yalianza muda mrefu kabla ya kuja kwa watawala wa Ulaya ambao kwa kiasi kikubwa wanaaminika kufika katika visiwa hivyo kwa usafiri wa boti ndogo ndogo maarufu kama kanuu ambazo zinaaminika kuwa zilitengenezwa na wakazi wa visiwa hivyo.

Zana mbalimbali za kufinyangwa zimekuwa zikipatikana katika visiwa vya Samoa na hata katika visiwa vya Marquesas zaidi ya kilometa elfu moja kutoka katika makao makuu ya Fiji.

Ukoloni hariri

Mpelelezi wa kutoka Uholanzi aliyejulikana kama Abel Tasman, aliitembelea Fiji katika miaka ya 1643, akiwa anatafuta bara la Afrika kusini lililojulikana kama “the great Southern continent”.

Kwa muda wa karne moja hivi iliyopita, katika visiwa vya Fiji kumekuwa kukiibuka tamaduni tofautitofauti, hali iliyooashiria ubaguzi wa kikabila kuwepo, tofauti na leo, ambapo, wakazi wa Fiji wamekuwa wakiishi kwa amani na wamekuwa wakikielezea kipindi hicho kama kipindi cha “na gauna ni tevoro” yaani "wakati wa shetani".

Baada ya uhuru hariri

Fiji ilijipatia uhuru wake kutoka katika utawala wa kikoloni wa Uingereza tarehe 10 Oktoba 1970.

Tangu uhuru katika visiwa vya Fiji kumekuwepo na mapinduzi ya kijeshi mara nne: mara mbili mwaka 1987, mara moja mwaka 2000, na mara moja mwaka 2006, lakini kwa ujumla, jeshi nchini humo limekuwa likishikilia madaraka ya moja kwa moja au kupitia kwa serikali iliyopo madarakani tangu mwaka 1987, hali iliyosababishwa na wakazi wa Fiji kulaumu serikali yao kutawaliwa na watu wenye asili ya Uhindi..

Mwaka 1990, katiba mpya katika utawala wa Fiji iliundwa ambayo ilichukua nafasi ya ile ya awali ambayo ilikuwa ikiegamia upande wa makabila kwa kiasi kikubwa.

Tarehe 10 Aprili 2009, Rais Iloilo, aliifuta katiba ya nchi hiyo na kufutilia mbali mamlaka ya mahakama akajitangaza kuwa rais wa visiwa hivyo, lakini baadaye alianzisha tena utawala wa kikatiba hali iliyopelekea mwenyewe kutolewa madarakani kwa kubainika alikuwa madarakani kinyume cha katiba.

Tarehe 13 Julai 2009, Fiji ilitolewa katika mkutano wa visiwa vinavopatikana katika bahari ya Pasifiki kutokana na kushindwa kwake kuendesha uchaguzi kwa njia ya kidemokrasia.

Hatimaye tarehe 17 Septemba 2014 uchaguzi huru ulifanyika na kukipa ushindi chama cha FijiFirst (59.2%).

  Makala hii kuhusu mambo ya kihistoria bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Historia ya Fiji kama enzi zake au matokeo yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.