Janette Deacon

Mwanaakiolojia wa Afrika Kusini

Janette Deacon (alizaliwa Cape Town, 25 Novemba 1939) ni mtaalam wa akiolojia wa Afrika Kusini aliyebobea katika usimamizi wa urithi na uhifadhi wa sanaa ya miamba. Amesomea mabadiliko ya zana za mawe kutoka maeneo ya kusini mwa Cape Town kuhusiana na mabadiliko ya hali ya hewa kwa miaka 20,000 iliyopita.[1][2] Kuanzia 1985, alipata maandishi ya mwamba mahali ambapo watoa habari wa / Xam Wilhelm Bleek na Lucy Lloyd waliishi katika karne ya 19. Alihudumu kama mshiriki wa Wakala wa Rasilimali za Urithi wa Afrika Kusini | SAHRA na alikuwa mwenyekiti wa kwanza wa Heritage Western Cape.

Janette Deacon
Amezaliwa 25 Novemba 1939
Cape Town
Nchi Bendera ya Afrika Kusini Afrika Kusini
Majina mengine Janette Deacon
Kazi yake mtaalam wa akiolojia

Maisha ya mwanzo na elimu hariri

Janette Buckland alisomea shule ya wasichana ya Rustenburg huko Cape Town kabla ya kuhitimu kutoka Chuo Kikuu cha Cape Town (UCT) mnamo mwaka 1960 na BA, ikifuatiwa na MA mnamo 1969 na PhD mnamo 1982 ambayo alichambua mkusanyiko wa baadhi wa zana za mawe (Stone Age) kutoka Pango la Nelson Bay, Pango la Boomplaas na makazi ya Kangkara.[3][4]

Kazi hariri

Baada ya kuhitimu BA yake alifanya kazi kama msaidizi wa utafiti wa WJ Talbot katika Idara ya Jiografia huko UCT.[5]na kuhadhiri katika Idara ya Akiolojia mnamo mwaka1962 na kutoka 1972 hadi 1975.[3]Kuanzia mwaka 1976 hadi mwaka 1988 alikuwa msaidizi wa utafiti katika Idara ya akiolojia katika Chuo Kikuu cha Stellenboschkutoka mwaka 1976 mpaka mwaka 1993[6]Amekuwa Katibu wa Heshima wa Jumuiya ya Archaeologist ya Afrika Kusini tangu mwaka 1997. Ndani ya mwaka 1989 aliteuliwa kama mtaalamu wa akiolojia katika National Monuments Council (Afrika Kusini na Namibia) | National Monuments Council (NMC), mpaka yeye alipostaafu mwaka 1999. Wakati huu aliwakilisha NMC katika Kikundi Kazi cha Sanaa na Utamaduni na timu ya uandishi wa Sheria Rasilimali za Urithi wa Kitaifa Namba 25 ya mwaka1999.

Baada ya kustaafu alikua mwenyekiti wa kwanza wa Heritage Western Cape (HWC) mnamo mwaka 2002 akihudumu hadi mwaka 2007[7]Kama katibu wa Mradi wa Sanaa ya Mwamba Kusini mwa Afrika, aliweka kozi na semina za uteuzi wa tovuti za sanaa za miamba kwenye Orodha ya Urithi wa Dunia. Kuanzia mwaka 1995 hadi mwaka 2011 mpango huu uliendelezwa zaidi kama mradi wa Getty Conservation Institute.

Mnamo 2016, alipewa udaktari wa heshima katika fasihi kutoka UCT kwa michango yake kwa akiolojia na utafiti wa sanaa ya miamba.[8]

Maisha binafsi hariri

Deacon aliolewa na Hilary Deacon, ambaye pia alifundisha archaeology katika Chuo Kikuu cha Stellenbosch, hadi kifo chake mnamo mwaka 2010.[9] Wana watoto watatu.[3]

Marejeo hariri

  1. Deacon, H.J., Deacon, J. 1999. Human beginnings in South Africa: uncovering the secrets of the Stone Age. Altamira Press.
  2. {{Cite news|url=http://www.timeslive.co.za/lifestyle/travel/2010/04/18/the-fossil-hunters-time-and-tides%7Ctitle=The Fossil Hunters: Time and Tides|last1=Vilakazi|first1=Nonhlanhla|date=18 April 2010|work=Times Live|last2=Inglis|first2=John|access-date=15 October 2016}}
  3. 3.0 3.1 3.2 "Janette Deacon". Stellenbosch Writers. Iliwekwa mnamo 15 October 2016.  Check date values in: |accessdate= (help)
  4. name=Xainki/>
  5. name=":0">"Janette Deacon". The African Rock Art Digital Archive. Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 5 October 2016. Iliwekwa mnamo 15 October 2016.  Unknown parameter |url-status= ignored (help); More than one of |archiveurl= na |archive-url= specified (help); More than one of |accessdate= na |access-date= specified (help); More than one of |archivedate= na |archive-date= specified (help); Check date values in: |archivedate=, |accessdate= (help)
  6. "UCT to Honour Leading Academics in African Art, Archaeology and Economics", University of Cape Town, 12 May 2016. 
  7. "Heritage Western Cape Celebrates 10th Anniversary". Western Cape Government. 29 October 2012. Iliwekwa mnamo 15 October 2016.  Check date values in: |date=, |accessdate= (help)
  8. "Janette Deacon - The Xainki, or Mother, of Archival Research", University of Cape Town, 15 June 2016. 
  9. "In Memoriam: Hilary John Deacon 1936–2010". South African Archaeological Bulletin 65 (191): 109–110. 2010. 
  Makala hii kuhusu mwanasayansi fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Janette Deacon kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.