Kanisa la Mtakatifu Clotilde

Kanisa la Mtakatifu Clotilde (maarufu kama: Basilique Ste-Clotilde) ni basilika la mjini Paris, linatokea katika maeneo ya Rue Las Cases, katika eneo la Saint-Germain-de-Pres. Kanisa hili linafahamika zaidi kwakuwa na minara miwili, yaani kulia na kushoto kote kuna minara.

Kanisa la Mtakatifu Clotilde jinsi linavyoonekana kwa mbele.

Historia ya kanisa la Mtakatifu Clotilde hariri

Ujenzi wa kanisa la basilica liliteuliwa lijengwe na Baraza kuu la Mji wa Parisi mnamo mwaka wa 1827. Lilisanifiwa na msanifu majengo F. C. Gau, kwa mtindo wa kizamani neo-Gothic (ujenzi wa Ulaya ya magharibi). Kazi ilianza mnamo mwaka 1846, ingawaje Gau alifariki mnamo mwaka wa 1853, lakini kazi iliendelezwa na Bw. Théodore Ballu ambaye alilimalizia kanisa hilo kabisa kunako mwaka wa 1857. Na likaja kufunguliwa mnamo tarehe 30 Novemba ya mwaka wa 1857 na Kadinali Morlot.

Wapigaji Kinanda wa Kanisa la Mtakatifu Clotilde hariri

Kanisa la Mtakatifu Clotilde linafahamika zaidi kwa wapiga vinanda wa kanisa hilo. Waliokuwa wapigaji kinanda maarufu wa kanisa hilo ni: