Kiluguru ni lugha ya Kibantu inayozungumzwa na Waluguru nchini Tanzania. Kufuatana na uainishaji wa lugha za Kibantu wa Malcolm Guthrie Kiluguru kiko katika kundi la G30.

Mwaka wa 2001 idadi ya wasemaji wa Kiluguru imehesabiwa kuwa watu 692,000. Lugha hii huzungumzwa hasa na Waluguru wanaopatikana katika mkoa wa Morogoro ambao ni wazawa. Sehemu maarufu kwa kuzungumzwa lugha hii ni: Matombo (inayojumuisha Tawa, Kibogwa, Milawilila, Uponda, Kitungwa, Konde, Kiswira), maeneo mengine ni tarafa ya Mgeta.

Mfano wa lugha: Hausindile maana yake Umeshindaje, Ukae maana yake Nyumbani, Imwana kolila maana yake mtoto analia.

Marejeo hariri

  • Maho, Jouni & Bonny Sands. 2002. The languages of Tanzania: a bibliography. (Orientalia et africana gothoburgensia, no 17.) Göteborg: Acta Universitatis Gothoburgensis. Pp ix, 428. ISBN 91-7346-454-6

Kitabu hiki kinataja marejeo mengine kama:

  • Mkude, Daniel J. 1974. A study of Kiluguru syntax with special reference to the transformational history of sentences with permuted subject and object. PhD thesis. University of London. Kurasa 335.

Viungo vya nje hariri

  Makala hii kuhusu mambo ya lugha bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Kiluguru kama historia yake, uenezi au maendeleo yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.