Liturujia ya Neno ndiyo sehemu kuu ya kwanza ya Misa, lakini inaweza kufanyika hata nje ya Misa kwa sababu kwa Wakristo Neno la Mungu ni lishe ya kwanza ya maisha ya Kiroho.

Askofu akihubiri mimbarini.

Mahali hariri

Katika makanisa kwa kawaida kuna mahali maalumu kwa ajili ya ibada hiyo, yaani mimbari, ambayo kwa sababu hiyo inaitwa pia "meza ya Neno".

Mbali nayo, altare inaitwa "meza ya Ekaristi" kwa kuwa ndipo mkate na divai vinapoombewa vishukiwe na Roho Mtakatifu ili viwe Mwili na Damu ya Kristo, ambavyo ndivyo chakula na kinywaji cha Wakristo.

Utaratibu hariri

Katika Kanisa Katoliki ni kawaida kusoma kwanza kutoka Agano la Kale, halafu kutoka Nyaraka za Mitume na hatimaye kutoka Injili mojawapo. Utaratibu huo unafuata ule wa utunzi wa maandiko hayo, ambapo ya mwisho ndiyo muhimu kuliko yaliyotangulia, kama katika historia ya wokovu ambapo Yesu ndiye aliyeleta divai bora mwishoni (Yoh 2:1-10).

Katikati kuna nyimbo, hasa Zaburi, ambazo zinaendana na masomo ya siku ili kuyaelewa, kuyatafakari, kuyaitikia na kuyashangilia.

Mara nyingi inafuata hotuba, halafu ungamo la imani na maombezi kwa ajili ya watu wote.

  Makala hii kuhusu dini ya Ukristo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Liturujia ya Neno kama historia yake, matokeo au athari zake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.