Ludoviko IX

(Elekezwa kutoka Louis IX)

Ludoviko IX (maarufu kama Mtakatifu Alois; Poissy, karibu na Paris, Ufaransa, 25 Aprili 1214Tunis, Tunisia, 25 Agosti 1270) alikuwa mfalme wa Ufaransa tangu 1226 hadi kifo chake.

Louis IX alivyochorwa na El Greco 15921595 hivi.
Sanamu ya Mt. Ludoviko IX huko Paris, Ufaransa.
Masalia yake yanatunzwa katika sanduku hili la mwisho wa karne ya 13 katika Basilika la Mt. Dominiko, Bologna, Italia.
Sanamu yake kama mwanajeshi katika Basilika la Moyo Mtakatifu, Paris.

Anahesabiwa kuwa mtawala bora wa Kikristo kwa jinsi alivyoishi kwa imani wakati wa amani na wakati wa vita alivyovipiga kwa nguvu zote ili kutetea Wakristo waliodhulumiwa, alivyojali ibada, msalaba, taji la miba na kaburi la Bwana, alivyotenda haki katika kuongoza nchi, alivyoheshimu ndoa yake na kulea vizuri watoto wake 11, alivyohudumia wananchi, hasa maskini na wagonjwa, na alivyovumilia matatizo yaliyompata [1].

Alifariki dunia kwa tauni aliyoambukizwa kwa kuwahudumia askari zake wakati wa vita vya msalaba.

Ni mfalme pekee wa nchi hiyo kutangazwa mtakatifu (na Papa Boniface VIII, 1297).

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe aliyoaga dunia[2].

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

Marejeo hariri

  • Davis, Jennifer R. "The Problem of King Louis IX of France: Biography, Sanctity, and Kingship," Journal of Interdisciplinary History Autumn 2010, Vol. 41, No. 2: 209–225. review of Gaposchkin (2008) and Le Goff (2009)
  • Gaposchkin, M. Cecilia. The Making of Saint Louis: Kingship, Sanctity, and Crusade in the Later Middle Ages (Cornell University Press, 2008) 352 pp.
  • Jordan, William Chester. Louis IX and the Challenge of the Crusade: A Study in Rulership (Princeton, 1979), a highly influential study says Davis (2010)
  • Le Goff, Jacques. Saint Louis (University of Notre Dame Press, 2009) 952 pp.

Viungo vya nje hariri

 
WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
  Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.