Magadi ni mji uliopo kando ya Ziwa Magadi upande wa mashariki, katika Bonde la Ufa la Afrika Mashariki. Pia mji wa Magadi upo kaskazini mashariki mwa Ziwa Natron in Tanzania.[1]

Mji wa Magadi upo kusini magharibi mwa Nairobi, kaskazini mashariki mwa Ziwa Natron nchini Tanzania (click map to enlarge)

Magadi ni kata ya Eneo bunge la Kajiado Magharibi, nchini Kenya[2].

Magadi ni makao makuu ya kaunti ndogo ya Magadi katika kaunti ya Kajiado. Kampuni ya Magadi Soda Company ipo katika mji huu.

Idadi ya watu wanaoishi Magadi ni 980 (sensa ya 1999) na kimo juu ya usawa wa bahari ni mita 595 [3]

Magadi imepata huduma za mtandao, na matumizi ya kompyuta, kwa njia ya Unite Nations Development Program-Kenya kwa ajili ya kompyuta zinazotumia nguvu ya jua. Mpango huu ulianza Julai 2002: na mwisho wa 2003, zaidi ya wakazi 10,000 (48%) walikuwa wametembelea vituo tano vya huduma za mtandao.[4]

Mji wa Magadi ulitumiwa katika filamu ya Fernando Meirelles ya The Constant Gardener.

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

  1. "FOUR DAYS - OLOGASAILE / MAGADI(BEAS 08)" (tour), Government of Kenya, 2006, BreakawayExpedition-Tour Archived 18 Oktoba 2006 at the Wayback Machine.
  2. Electoral Commission of Kenya: Registered voters per polling station by electoral area/ward and constituency Archived Septemba 29, 2007, at the Wayback Machine
  3. "Magadi, Kenya Page" (statistics), Falling Rain Genomics, Inc., 2004, FallingRainCom-Magadi.
  4. "Community Solar Powered E-Centers, Magadi, Kenya" (computer access), United Nations Development Programme, 2004, UNDP-Solar-Magadi Archived 21 Aprili 2005 at the Wayback Machine..

Viungo vya nje hariri

Coordinates: 1°53′S 36°16′E / 1.883°S 36.267°E / -1.883; 36.267