Majadiliano:Koitalel Arap Samoei


JABALI KOITALEL

..na Baroswa Francis araap Talam mwandishi wa “KOITALEL SAMOEI NANDI FOUNDATION”

Dau la kusafiria wanandi kabla ya kufika kwa wakoloni Kenya aliitwa koitalel kimanyei Barbarani samoei araap Turugat. Alizaliwa mnamo mwaka wa 1850 katika kitongoji cha samitui-aldai wilayani nandi kusini.Babake aliitwa kipnyolei Turugat na mamake alikuwa Taprat-or chebo kap leu.Ndugu zake walikuwa:kipchomber arap koilegei,kibuigut kipng’etich araap Boisio na siratei araapsimbolei. Wanandi walimtia katika kumbukumbu na taadhima koitalel kutokana na staha na vipaji vingi vilivyopigia mbiu ya sifa;Alipokuwa na umri ya makamo.sadfa kubwa ilikuwa ni jina lake lenye viunganishi ya maneno mawili:KOITA-Lina maan-mwamba na lel linamaanisha –eupe pe! Lisilokuwa na dozari. Wakati moja koitalel alionyesha hayo kwa kushinda kaka zake kwa kupita mtihani ya baba yao kipnyolei. Aliweza kutoa maana ya tabiri alipoona wazungu wakija katika nchi ya Nandi na mambo mengine ambayo yamehifadhiwa na wazee.kule Kupita kwake kulipelekea kupendwa na kuchaguliwa na wanandi. Makazi yake yalikuwa: viunga vya chuo cha moi,kapsimotwa na baadaye kipkimba (cheboin). Alioa wake sita ambao walikuwa: 1. kobot chepsielei 2. Tabarchok chebo chebwai 3. Tabololei chebo kamirmet 4. Tabrongoei chebo chemwaan 5. Tamiron chebochelimet Chini ya pendera yake,alichemshwa roho na kufika kwa wakoloni.alipigana jino na meno kwa zaidi ya miaka kumi na moja (vitabu vingi vina uongo ya kuonyesha picha ya kushindwa kwa wanandi kwa muda mfupi);kutoka mwaka wa 1894 hadi 1905 aliouwawa kikatili na Richard meinertzhagen.Alipigwa chuku ya ‘kuja tutafanya amani na baadaye kuaga buriani na hayati: 1. kibitz kut araap chemurungu 2. manyinya 3. kip bek kelek 4. araap sato 5. kesween araap butia 6. arap sirtui Chambilecho wasemaji “kuutia msumari kwenye kidonda au kuchokoza nyuki” vita ya ukombozi zilichacha. kuuwawa kwa koitalel kulizua shari kati ya wanandi na wakoloni.Hii ilipelekea jamii ya koitalel kusakwa kama adui,kutekwa nyara na kupelekwa kizuizini kapsisiywo mwaka wa 1918.kule ni kisiwa kidogo kilichokuwa na mbu wakali.mmoja ya vijana wa koitalel aliiweka mwenge ya baba yake juu kwa kufungwa miaka yapata arobaini.Huyo aliitwa BARSIRIAN ARAAP MANYEI.(alifungwa nyeri,muranga,kapsabet na gwasi) Wengine waliotiwa kizuizini walikuwa: 1. Barsirian araap manyei 2. kiptololet araap lelimo 3. kipsaina araap samoei 4. koringo araap manyei 5. kinaa araap koitalel 6. kipnyolei araap ng’erer bei 7. Baasi rongoei araap tekentany 8. kipng’etich araap menei 9. chepkwony araap matutu 10. kirwa araap chepkwony 11. kibinot araap rongoei 12. kimulot araap chepkwony

Rudi kwenye ukurasa wa " Koitalel Arap Samoei ".