Majadiliano:Orodha ya shule nchini Tanzania

Latest comment: miaka 4 iliyopita by Kipala

Orodha hii ni ya lini? Kwa mfano, usajiri Alfagems Secondary School ni wa mwaka 2008, lakini haimo. --Riccardo Riccioni (majadiliano) 04:11, 26 Februari 2017 (UTC)Reply

Uzuri wa Wikipedia, unachokiona hakipo, unaongezea! Hata shule ya msingi Kiwalani haijakuwepo - mahali ambapo mimi nimesoma. Shule ya Yombo na Kiwalani ni shule ambazo zipo tangu sabiini mwanzoni... Nimeongeza kwenye orodha. Hata wewe unaweza mkuu...Ndiyo dhumuni hasa--MwanaharakatiLonga 11:15, 26 Februari 2017 (UTC)Reply
Si vibaya kuorodhesha shule - ingawa kama unataka pia shule za msingi unapaswa kuunda orodha za wilaya au tarafa! Hata hivyo naomba tusiendelee kuunda makala kuhusu kila shule maana hapa tunapata tatizo la Wikipedia:Umaarufu, ambayo haipatikani kwa shule nyingi.
Tufuate mashariti ya kimsingi ya umaarufu, kama vile Wikipedia:Umaarufu#Kanuni_ya_kimsingi_kuhusu_umaarufu_kwenye_Wikipedia:
  • Mada (au mtu) inastahili makala kama masharti matatu yanatimizwa:
    • imeshajadiliwa katika jamii kwa kiwango fulani (si mara ya kwanza hapa wikipedia!)
    • katika vyanzo vinavyoweza kutegemewa (si facebook, twita, tovuti ya binafsi tu)
    • tena vyanzo visivyotungwa na wenyewe (si tovuti ya wenyewe, matangazo yao).
Maana kama hatuna ushuhuda nje ya facebook au tovuti ya wenyewe au kutajwa kwa jina tu katika orodha fulani - hatuna umaarufu wa kutosha. Nashauri tusiendelee kuunda makala hizi pasipo na ushuhuda imara zaidi. Kipala (majadiliano) 19:07, 21 Agosti 2019 (UTC)Reply
Rudi kwenye ukurasa wa " Orodha ya shule nchini Tanzania ".