Maporomoko ya Kalambo
Maporomoko ya Kalambo yanatokana na mto Kalambo ambao ni mpaka wa Tanzania na Zambia.
Maporomoko ya maji hayo, ukiachilia kuwa ni ya pili baada ya yale ya Tugela (Afrika ya Kusini), lakini pia ndiyo maporomoko pekee yanayogawa nchi mbili.
Maporomoko hayo yapo katika kijiji cha Kapozwa, kata ya Kisumba, Wilaya ya Kalambo, Mkoa wa Rukwa. Katika kijiji cha Kapozwa, ambacho kilianzishwa kutokana na imani kuwa ukienda kuoga katika maporomoko hayo utapooza. Kwa kuambiwa hivyo wenyeji wa eneo hilo walipaita kijiji jina la Kapozwa.
Maporomoko hayo yamekuwa yakionekana na kutangazwa kuwa yapo Zambia na hivyo kuiondoa Tanzania kuwa miongoni mwa nchi zenye maporomoko yanayotambulika duniani.
Marejeo hariri
Viungo vya Nje hariri
- Maporomoko ya kalambo Archived 9 Januari 2010 at the Wayback Machine.
- Kalambo Archived 5 Machi 2010 at the Wayback Machine.
Makala hii kuhusu maeneo ya Tanzania bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Maporomoko ya Kalambo kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. Usitaje majina ya madiwani na viongozi au maafisa wengine wa sasa maana wanabadilika haraka mno. |