Maria wa Bethania (jina lake kwa Kiebrania מִרְיָם, Miryām, kwa Kiaramu מרים, Maryām, kwa Kigiriki Μαρία, Maria) alikuwa mwanamke wa Bethania, kitongoji cha Yerusalemu, katika karne ya 1[1].

Kristo nyumbani mwa Martha na Maria kadiri ya mchoro wa Johannes Vermeer (1654 hivi) unaotunzwa kwenye National Gallery of Scotland, Edinburgh. Maria ameketi miguuni pa Yesu.
Mfululizo wa kurasa juu ya Yesu
Jesus
Yesu Kristo na Ukristo

Umwilisho  • Utoto wa Yesu  • Ubatizo
Arusi ya Kana • Utume wa Yesu • Mifano ya Yesu  • Miujiza ya Yesu
Kugeuka sura • Karamu ya mwisho • Msalaba wa Yesu  • Maneno saba
Kifo cha Yesu  • Ufufuko wa Yesu
Kupaa mbinguni  • Ujio wa pili
Injili  • Majina ya Yesu katika Agano Jipya  • Yesu kadiri ya historia  • Tarehe za maisha ya Yesu • Kristolojia

Mazingira ya Yesu

Wayahudi • Kiaramu • Bikira Maria • Yosefu (mume wa Maria) • Familia takatifu • Ukoo wa Yesu • Ndugu wa Yesu • Yohane Mbatizaji

Mitazamo juu ya Yesu

Mitazamo katika Agano Jipya · Mitazamo ya Kikristo • Mitazamo ya Kiyahudi • Mitazamo ya Kiislamu • Yesu katika sanaa

Ndugu zake walikuwa Martha na Lazaro wa Bethania, ambao wote Yesu alifurahia urafiki wao hasa alipohiji kwenda Yerusalemu.

Wanaheshimiwa na Wakristo wengi kama watakatifu[2].

Sikukuu yao inaadhimishwa pamoja tarehe 29 Julai[3] au 4 Juni, kadiri ya madhehebu.

Maisha hariri

Anajulikana hasa kutokana na Injili, kwa namna ya pekee Injili ya Luka (10:38-42) na Injili ya Yohane (11; 12:1-8), katika Agano Jipya ndani ya Biblia ya Kikristo.

Humo anaonekana mwenye silika ya utulivu na imani kwa Yesu Kristo, ambaye alipendezwa sana na usikivu wake wakati alimfundisha ameketi chini karibu na miguu yake, kama ilivyokuwa kawaida ya wanafunzi wa dini ya Kiyahudi, ingawa wakati huo wanaume tu walikubalika.

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

Viungo vya nje hariri

  Makala hii kuhusu mtu wa Biblia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Maria wa Bethania kama habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.