Mdumu-mwitu
Mdumu-mwitu (Sarracenia flava)
Mdumu-mwitu (Sarracenia flava)
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Plantae (Mimea)
(bila tabaka): Angiospermae (Mimea inayotoa maua)
(bila tabaka): Eudicots (Mimea ambayo mche wao una majani mawili)
Oda: Caryophyllales/Ericales (Mimea kama fungu/mdambi)
Familia: Nepenthaceae/Sarraceniaceae (Mimea iliyo na mnasaba na mdumu-mwitu)
Ngazi za chini

Jenasi 5:

Midumu-mwitu ni mimea inayokula wadudu kwa kutumia mtego kwa umbo wa kikombe kirefu au mdumu wenye maji ndani. Mimea hii ni wana wa familia mbili: Nepenthaceae au midumu-mwitu ya Dunia ya Kale na Sarraceniaceae au midumu-mwitu ya Dunia Mpya (familia Cephalotaceae ina spishi moja tu). Imedhaniwa kuwa mitego ya midumu-mwitu yenye maji ndani iliibuka kutoka matawi yaliyojikunja, huku mabadiliko ya viumbe yakipendelea matawi yenye michimbuko mikubwa zaidi katika kipindi cha miaka mingi.

Hata hivyo, baadhi ya midumu-mwitu wa jenasi kama ile ya Nepenthes wanajumuishwa katika kikundi tofauti cha mimea wenye matawi kama karatasi yenye gundi. Hili linaonyesha kuwa mtazamo kuwa midumu mwitu iliibuka kutoka matawi yaliyojikunja huenda hukawa si wa kweli.

Bila kujali jinsi mmea huu ulivyobadilika, wadudu wanaotambaa na wanaoruka ikiwemo nzi huvutiwa kwa mchimbuko huo ulioundwa na tawi, mara nyingi kwa rangi na maji yenye sukari. Pande za tawi huenda zikawa zinateleza na zimeumbwa kwa njia inayowafanya wadudu washindwe kutoka pindi wanapoingia ndani.

Picha hariri

Marejeleo zaidi hariri

  • Schnell, Donald (2003). Carnivorous Plants of the United States and Canada. Second Edition. Timber Press, Oregon, U.S.A.
  Makala hii kuhusu mmea fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mdumu mwitu kama uainishaji wake wa kibiolojia, uenezi au matumizi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.