Michael Ranneberger

Michael E. Ranneberger ndiye Balozi wa Marekani wa sasa nchini Kenya. Alithibitishwa na bunge tarehe 29 Juni 2006 na kuanza kazi moja kwa moja mnmao 11 Agosti 2006. Yeye pia ana wajibu kwa uhusiano wa Marekani na Somalia. Mheshimiwa Ranneberger alihudumu kama Mwakilishi mkuu wa Sudan katika Taasisi ya Masuala ya Afrika kuanzia Januari hadi Agosti mwaka wa 2006. Kuanzia mwaka wa 2004 hadi mwaka wa 2005, alikuwa Naibu Katibu Msaidizi Mkuu wa Taasisi ya Afrika (kwa lugha ya Kimombo ‘Africa Bureau’). Aliwahi kuhudumu kama Mshauri Maalum wa Sudan kuanzia mwaka wa 2002 hadi mwaka wa 2004. Kuanzia mwaka wa 1999 hadi mwaka wa 2002, alikuwa Balozi wa Marekani katika Jamhuri ya Mali. Yeye ni mwanachama wa Huduma Kuu ya Kigeni na anashikilia nyadhifa ya Waziri wa wasifu (Career Minister).

Michael E. Ranneberger

Kuanzia Julai mwaka wa 1995 hadi Julai mwaka wa 1999, kama Mratibu wa maswala ya Kuba, Bw. Ranneberger alisaidia kuongoza sera ya Utawala ili kukuza mpito wa amani wa kidemokrasia katika nchini Kuba, na kwa sehemu yake aliimarisha msaada kwa wanaharakati wa haki za binadamu na maendeleo ya jamii ya raia inayojitegemea. Mara moja kabla ya kuchukua nyadhifa hiyo ya Kuba, kwa miezi sita alikuwa nchini Haiti akianzisha na kuendesha shirika la Haki na Maswala yanayohusiana na Usalama.

Mnamo Agosti mwaka wa 1994, akawa Naibu Mkuu wa Misheni katika mji mkuu wa Mogadishu. Huduma yake kama Naibu Mkuu wa Misheni katika mji mkuu wa Maputo kuanzia mwaka wa 1986 hadi mwaka wa 1989 ilijumuisha miezi nane kama mjukumu wakati wa vita vya wenyewe kwa wenyewe, wakati mpango wa msaada wa dharura wa Shirika la Maendeleo ya Kimataifa la Marekani,(USAID) nchini Msumbiji ulikuwa mmoja wa mpango kubwa zaidi katika sub-Saharan ya Afrika. Kama ofisa wa dawati nchini Angola kuanzia mwaka wa 1981 hadi1984 alihudumu kama mwanachama wa Katibu Msaidizi wa timu ya Crocker katika mazungumzo ya kuleta uhuru katika nchi ya Namibia na kuondolewa kwa vikosi vya Kuba nchini Angola.

Kuanzia mwaka wa 1989 hadi mwaka wa 1992 alihudumu kama Naibu Mkuu wa Misheni katika Asuncion, ambapo alihusika katika kusaidia mpito wa kidemokrasia wa baada ya Stroessner. Alipokuwa anashikilia nyadhifa ya Naibu Mkurugenzi wa Masuala ya Amerika ya Kati kuanzia mwaka wa 1992 hadi mwaka wa1994 alisaidia kusimamia utekelezaji wa mikataba ya amani nchini El Salvador na juhudi za kumaliza migogoro ya ndani nchini Guatemala. Baada ya kuhudumu kama msaidizi Maalum Katibu kuanzia mwaka wa 1984 hadi mwaka wa 1985, alituzwa tuzo la Ushirika wa Masuala ya Kimataifa katika Baraza ya Mahusiano ya Nje.

Bw Ranneberger alipata BA(shahada ya sanaa) kutoka Chuo Kikuu cha Towson State huko Baltimore na MA katika historia kutoka Chuo Kikuu cha Virginia. Yeye ni mpokeaji wa Heshima Awards Superior saba kutoka Idara na Rais Meritorious Service Award.

Marejeo hariri

  This article incorporates public domain material from the United States Department of State document "Michael E. Ranneberger".