Mkurugenzi (kwa Kiingereza: director) ni kiongozi wa juu kabisa katika utawala wa kampuni au taasisi yoyote.

Mkurugenzi

Wakurugenzi Wakuu hutafuta kazi katika mashirika mbalimbali, yakiwemo mashirika ya umma na yale ya binafsi, mashirika yasiyolenga faida, na hata baadhi ya mashirika ya serikali (hasa kampuni za serikali). Katika sekta isiyo ya kifaida na zile za serikali, Wakurugenzi Wakuu kwa kawaida hulenga kufikia matokeo yanayohusiana na dhamira ya shirika husika, ambayo kwa kawaida huwa ni kwa mujibu wa sheria. Wakurugenzi Wakuu pia mara nyingi hupewa jukumu la meneja mkuu wa shirika na afisa wa cheo cha juu zaidi katika shirika ama kampuni husika.[1]

Mkurugenzi Mtendaji wa shirika au kampuni kwa kawaida huripoti kwa bodi ya wakurugenzi na mara nyingi kazi yao kubwa huwa ni kuongeza thamani ya biashara kwa kampuni waliyoajiriwa nayo ambayo inaweza kujumuisha kuongeza bei ya hisa, sehemu ya soko, mapato au kipengele kingine chochote.

Marejeo hariri

  1. Westphal, James D.; Zajac, Edward J. (1995). "Who Shall Govern? CEO/Board Power, Demographic Similarity, and New Director Selection". Administrative Science Quarterly 40 (1): 60–83. ISSN 0001-8392. doi:10.2307/2393700. 
  Makala hii kuhusu mambo ya uchumi bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkurugenzi kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.