Mshtarii ni sayari ya tano kutoka Jua katika Mfumo wa Jua, na sayari kubwa kabisa ya mfumo. Tungamo yake inazidi mara mbili na nusu masi ya sayari nyingine zote pamoja.

Mshtarii
Picha ya Mshtarii iliyopigwa na Darubini ya Angani ya Hubble mnamo 2014.
Picha ya Mshtarii iliyopigwa na Darubini ya Angani ya Hubble mnamo 2014.
Jina
Asili ya jinaKar. المشتري (al-mushtari)
Majina mengine
Mshitari, Mshiteri, Mshatira
Jupiter/Jupita (Kng.)
Alama♃
Tabia za njiamzingo
Umbali mfupikm 740,595,000
au 4.9506
Umbali mrefukm 816,363,000
au 5.4570
km 778,479,000
au 5.2038
Uduaradufu0.0489
siku 4,332.59
miaka 11.862
Mwinamo1.303° toka njia ya Jua
Miezi95
Tabia za gimba
km 69,911
Tungamokg 1.8982×1027
mara 317.8 ya Dunia
g/cm3 1.326
Uvutano wa usoni
m/s2 24.79
saa 9.9258
saa 9.9250
Weupe0.503 (Bond)
0.538 (jiometri)
HalijotoK 165 (−108.15°C)

Angahewa

Mshtarii haina uso unaoonekana. Sehemu kubwa ya tungamo ya sayari ni elementi nyepesi kama hidrojeni na heli ambazo ni gesi katika mazingira ya duniani. Hii ndiyo sababu ya kwamba sayari kubwa za Mshtarii pamoja na Zohali huitwa "sayari jitu za gesi".

Kadiri gesi hizo zinavyopatikana chini zaidi (yaani kuelekea ndani) uzito wa matabaka ya juu unaongeza shinikizo katika vilindi vyake na kusababisha gesi za angahewa kuingia katika hali ya giligili (majimaji) inayobadilika kuwa mango ndani zaidi. Zamani iliaminika ya kwamba sayari yote ni ya gesi iliyoganda lakini siku hizi wataalamu wa anga huamini kwamba kuna kiini cha mwamba au metali.

Doa jekundu linaloonekana usoni mwa angahewa ni dhoruba ya tufani kubwa sana iliyotazamwa tangu darubini za kwanza zilipopatikana. Duniani tufani zinapotea kwa kawaida baada ya wiki kadhaa lakini doa jekundu limeendelea bila kusimama kwa miaka 300.

 
Ulinganishi wa ukubwa wa Dunia yetu (kushoto) na Mshtarii pamoja na "doa jekundu" inayozunguka katika angahewa ya Mshtarii.

Miezi

Mshtarii ina miezi 79 iliyotambuliwa hadi mwaka 2018[1].

Miezi minne mikubwa ilitambuliwa mwaka 1610 na Galileo Galilei aliyekuwa kati ya wanaastronomia wa kwanza kutumia darubini. Ndiyo Io, Europa, Ganimedi na Kalisto. Ukubwa wa Ganimedi unakaribia kipenyo cha Utaridi ukipita kile cha Pluto. Miezi 63 huwa na kipenyo chini ya kilomita 10. Mwezi mdogo kabisa wa Mshtarii unajulikana kwa namba tu na una kipenyo cha km 1.

Marejeo

  1. Sheppard, Scott S.. The Giant Planet Satellite and Moon Page. Department of Terrestrial Magnetism at Carnegie Institution for Science. Jalada kutoka ya awali juu ya June 7, 2009. Iliwekwa mnamo December 19, 2014.
  Makala hii kuhusu mambo ya sayansi bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mshtarii kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.