Nembo ya Uganda imetengenezwa na ngao na mikuki miwili kwenye mlima wenye rangi kijani.


Ngao na mikuki vinawakilisha utayari wa watu wa Uganda katika kutetea nchi yao. Kuna taswira tatu juu ya ngao hii: ya juu inawakilisha mawimbi ya Ziwa Victoria; jua lililopo katikati linawakilisha siku nyingi za mwanga mzuri wa jua ambao Uganda inafurahia; na ngoma ya jadi chini ni mfano wa dansi, na mayowe ya watu kwenye mikutano na hafla.

Upande wa kulia ngao imepakana na Crested Crane (Balearica regulorum gibbericeps), ambayo ni moja ya uzao wa Grey-crowned Crane na ndege wa taifa wa Uganda. Upande wa kushoto ni Kob wa Uganda (Kobus kob thomasi), ambaye ni aina ya Kob na hapa anawakilisha wingi wa wanyamapori.

Ngao imesimama kwenye mlima wa kijani, kuwakilisha ardhi yenye rutuba, na moja kwa moja juu ya uwakilishi wa Mto Nile. mazao makuu mawili ya biashara ambayo ni kahawa na pamba yapo pembezoni mwa mto huu. Chini ni mbiu ya taifa: "Kwa ajili ya Mungu na nchi yangu".

Angalia pia hariri