Ngoma (muziki)

music genre

Ngoma inaweza kumaanisha muziki unaochezwa na ala ya muziki inayoitwa ngoma pia.

Ngoma (djembe)

Ngoma ni muziki na lugha ya pekee inayotumika kwa kuelezea utamaduni na historia ya nchi fulani, tunatumia lugha ya ngoma katika kuelezea hali mbalimbali za maisha yetu, kama vile huzuni, furaha, mapenzi, faraja, vitisho, shukurani na ushindi.

Tangu zamani Waafrika walikuwa na lugha hii ya ngoma ambayo ilirithishwa kwa mapokeo.

Ngoma pia ilitumika na jamii mbalimbali kama njia ya kuita watu kwenye kusanyiko muhimu, kama vile vita, mikutano n.k. na ilipigwa kwa milio tofauti kulingana na tukio.

Makala hii kuhusu mambo ya muziki bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Ngoma (muziki) kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.