Kwa maana nyingine ya neno "Niger" tazama Niger (maana)

Niger
Ramani ya Niger.

Niger (pia Nijeri) ni nchi kubwa zaidi ya Afrika ya Magharibi kwa eneo, lakini 80% ni katika jangwa la Sahara.

Imepakana na Algeria na Libya upande wa kaskazini, Mali na Burkina Faso upande wa magharibi, Chad upande wa mashariki na Nigeria pamoja na Benin upande wa kusini.

Mji mkuu ni Niamey, kusini mwa nchi.

Jiografia hariri

Niger haina pwani kwenye bahari yoyote.

Ni sehemu ya kanda la Sahel, yaani sehemu kubwa ya nchi ni yabisi, kaskazini mwake ni yabisi sana ikiwa jangwa la Sahara.

Ardhi yenye rutuba iko kusini kabisa, karibu na mto wa Niger.

Historia hariri

Jaribio la mapinduzi lilifanyika usiku wa kuamkia Machi 31, 2021, siku chache kabla ya kuapishwa kwa Mohamed Bazoum, rais mteule.

Mnamo Aprili 2, 2021, Mohamed Bazoum aliapishwa na kuchukua madaraka.

Watu hariri

Mipaka ilichorwa wakati wa ukoloni wa Ufaransa, ikiunganisha watu wenye utamaduni tofautitofauti, kama vile Watuareg (9.3% za wakazi wote) wa Sahara, wahamaji Wafula (8.5%) na Wakanuri (4.7%) wa eneo la Sahel na wakulima wa kusini kama Wasonghai (21%) na Wahausa: hawa wa mwisho ni 55.4% .

Tofauti hizo kubwa zilileta kipindi cha ugomvi kati ya makabila uliopoa tena baada ya mwaka 2000. Tatizo kubwa la nchi ni vipindi vya ukame na njaa vinavyorudiarudia mara kwa mara.

Wakazi walikuwa zaidi ya milioni 17 katika sensa ya mwaka 2012. Kwa sasa ni 22.4 kutokana na ongezeko la haraka. Idadi kubwa wako kusini.

Kadiri ya utafiti wa mwaka 2005, asilimia 8 walikuwa watumwa.

Tangu wakati wa ukoloni, lugha rasmi ni Kifaransa. Lakini kuna lugha 10 za taifa kati ya lugha kuu za makabila asili. Muhimu zaidi ni Kihausa na Kizarma-Sonrai.

Walio wengi kabisa (99.3%) ni wafuasi wa Uislamu; baadhi yao wanasemekana kuchanganya Uislamu na dini asilia za Kiafrika. Wakristo ni 0.3% tu. Hata hivyo Niger ni nchi isiyo na dini rasmi.

Tazama pia hariri

Viungo vya nje hariri

 
WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:


Nchi za Afrika  
Afrika ya Kati (Jamhuri ya) | Afrika Kusini | Algeria | Angola | Benin | Botswana | Burkina Faso | Burundi | Cabo Verde | Chad | Cote d'Ivoire | Eritrea | Eswatini | Ethiopia | Gabon | Gambia | Ghana | Guinea | Guinea Bisau | Guinea ya Ikweta | Jibuti | Kamerun | Kenya | Komori | Kongo (Jamhuri ya) | Kongo (Jamhuri ya Kidemokrasia ya) | Lesotho | Liberia | Libya | Madagaska | Malawi | Mali | Misri | Morisi (Visiwa vya) | Mauritania | Moroko | Msumbiji | Namibia | Niger | Nigeria | Rwanda | Sahara ya Magharibi | Sao Tome na Principe | Senegal | Shelisheli | Sierra Leone | Somalia | Sudan | Sudan Kusini | Tanzania | Togo | Tunisia | Uganda | Zambia | Zimbabwe
Maeneo ya Afrika ambayo ni sehemu za nchi nje ya Afrika
Hispania: Kanari · Ceuta · Melilla | Italia: Pantelleria · Pelagie | Ufaransa: Mayotte · Réunion | Uingereza: · St. Helena · Diego Garcia | Ureno: Madeira
  Makala hii kuhusu maeneo ya Afrika bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Niger kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.