Noah Kiprono Ngeny (amezaliwa 2 Novemba 1978) ni mwanariadha wa Kenya na mshindi wa kiajabu wa mita 1500 katika mashindano ya Olimpiki ya 2000.

Rekodi za medali
Riadha ya Wanaume
Anawakilisha nchi Bendera ya Kenya Kenya
Mashindano ya Olimpiki
Dhahabu 2000 Sydney 1500 m
Mashindano ya Dunia ya IAAF
Fedha 1999 Sevilla 1500 m

Kazi yake hariri

Kabla ya Sydney hariri

Ngeny anatoka kijiji cha Kabenes katika eneo la Kipsangui, Tarafa ya Ziwa wilayani Uasin Gishu nchini Kenya [1].

Alicheza Voliboli wakati wa enzi zake za shule na hakuanza kukimbia hadi 1996[2].

Alikuja kujulikana duniani baada ya kuweka rekodi mbili za wanariadha Chipukizi mnamo 1997 – 3:32:91 kwa mita 1500 jijini Monaco na 3:50:41 kwa shindano la Mile kule Nice. Wakati huu alikuwa chini ya ukufunzi wa meneja maarufu na koja marehemu Kim McDonald. Mnamo 1998 aliiboresha rekodi yake ya 1500 kuwa 3:30:34 kule Monaco.

Mnamo Julai 1999 jijini Roma, Ngeny alimaliza wa pili nyuma ya El Guerrouj huku El Guerroujakiweka rekodi ya dunia (3:43:13) kwa shindano la kukimbia maili moja. Ngen alimkaribia hadi tofauti ya 0:00:27 akimaliza kwa muda wa 3:43:40, bado rekodi ya pili na sekunde moja juu ya rekodi iliyopita ya 3:44:39 iliyokuwa imewekwa na Noureddine Morceli.[3][4] Mnamo 24 Agosti 1999 Ngeny aliinyakua medali ya Fedha (3:28:73) katika mbio za mita 1500 katika Mashindano ya Dunia ya IAAF yaliyoandaliwa na Seville, Uhispania. Mashindano hayo yalishindwa na Bingwa wa Duunia Hicham El Guerrouj wa Morocco (3:27.65) [5] .

Mnamo 5 Septemba 1999, Ngeny aliweka rekodi ya sasa ya Dunia ya 2:11:96 katika umbali wa mita 1000 kule Rieti, Italia, akivunja rekodi iliyokuwa imeshikiliwa kwa miaka 18 na Sebastian Coe tangu 1981. Muda wa Ngeny wa 2:11:96 bado ndio muda bora zaidi duniani na hakuna mwanariadha yeyote amewahi kuukaribia kwa chini ya sekunde mbili[6]. Rekodi aliyoivunja iliwahi kuwa rekodi iliyoshikiliwa kwa muda mrefu zaidi, Pia ilikuwa rekodi ya pekee ya masafa yoyote ya kukimbia ambayo ilikuwa haijawahi kushikiliwa na mwanariadha wa asili ya Kiafrika[2]. Katika mwaka wa 1999 Ngeny aliandikisha muda kati ya 3:30 mara sita katika shindano la Mita 1500 na akajiimarisha kama mpinzani wa karibu zaidi wa bingwa wa Dunia Hicham El Guerrouj.

Mnamo 11 Agosti 2000, Ngeny alimaliza wa pili katika mashindano ya Weltklasse Zürich katika mbio za mita 1500 (3:27.21) na kuwa mwanariadha wa Kenya ambaye anashikilia [[|Rekodi za Kenya za Riadha|rekodi ya Kenya]] na wa tatu wa kasi zaidi katika mbio hizo. Hatimaye rekodi hii ilivunjwa na Benard Lagat (3:26.34) jijini Bruxelles mnamo 2001, 24 Agosti. Lagat aliandikisha rekodi hiyo wakati alipomaliza wa pili nyuma ya Hicham El Guerrouj (3:26.12) [7]

Ushindi Jijini Sydney hariri

Ngeny Ashinda katika Olimpiki jijini Sydney
Ngeny Ashinda katika Olimpiki jijini Sydney

Mnamo 29 Septemba 2000, katika fainali za mita 1500 wakati wa Michezo ya Olimpiki wa 2000 jijini Sydney Australia, Ngeny alimshinda bingwa wa Dunia na anayeshikilia rekodi ya Dunia mara mbili Hicham El Guerrouj ambaye alikuwa hajawahi kushindwa na alipigiwa upato nawengi kushinda. Ngeny alimpita katika mita 100 za mwisho[8] [9] .[10] Wakati huo huo Ngeny aliweka rekodi mpya ya Olompiki ya 3:32.07, akivunja ile ya Sebstian Coe ya 3:32:53 mnamo 1984. . Hicham El Guerrouj aliangukia Fedha katika shindano hilo kwa muda wa 3:32.32 na mwenzi wa Ngeny Benard Lagat ambaye sasa ni raia wa Marekani akashinda shaba kwa muda wa 3:32.44. Noa Ngeny alikuwa mkenya wa Kwanza kushinda taji la mita 1500 akifuata Kipchoge Keino katika mashindano ya Olimpiki ya 1968 jiini Mexico na Peter Rono katika mashindano ya Olimpiki ya 1988 jijini Seoul.

Mwaka huo ulikuwa kilele cha kazi yake ya riadha. Alieka muda bora zaidi katika kazi yake wa 1:44:49 kwa mita 800 (28 Julai jijini Oslo) na 3:28:12 kwa mita 1500 kule Weltklasse Zürich (11 Agosti) kuelekea ushindi wake katika Olimpiki (29 Septemba).

Muda bora zaidi katika kazi yake ni 3:28.12 jijini Zürich na unamfanya mwanariadha wa nne wa kasi zaidi wa mita 1500, nyuma ya Hicham El Guerrouj, Bernard Lagat, na Noureddine Morceli.

Baada ya Sydney hariri

Ngeny alitolewa katika timu ya Kenya wakati wa Mashindano ya Ubingwa wa Dunia kule Edmonton baada ya kukaidi maagizo ya Shirikisho la Riadha nchini kurejea nyumbani kutoka Uingereza anakofanyia Mazoezi[11].

Huku El Guerrouj akishinda mashindano ya Dunia ya 2003, Ngeny hangeweza kufuatilia mafanikio yake ya 2000, kutokana na ajali ya gari.

Alirejea nchini Australia mnamo 2001 huku akishinda mashindano ya ‘’Goodwill’’ ya Maili jijini Brisbane lakik=ni ajali ya gari nchini Kenya mwezi wa Novemba ilimpumzisha kutoka riadha kwa msimu huo wote. Maumivu aliyoyapata yaliidhuru kazi yake tangu hapo. Hakushiriki mashindano mengi kati ya 2003 hadi 2004 lakini aliweka muda bora zaidi wa 3:33:38 lakini akashindwa kufuzu kwa mashindano ya Olimpiki katika timu ya Kenya kwa hivyo hangeweza kulitetea taji lake mjini Athens. Ngeny hakushiriki katika majaribio ya Kenya ya Mashindano ya Dunia ya 2003 kwa sababu ya Maumivu[12] [13].

Kustaafu hariri

Alitangaza kustaafu kwake rasmi kutoka riadha ya akimataifa mnamo 22 Novemba 2006[14]. Ngeny anajivunia matokeo yake mnamo 2000 wakati wa Mashindano ya Olimpiki jijini Sydney.

Muda Bora zaidi hariri

Masafa Muda Tarehe Mahali
800 m 1:44.49 28 Julai 2000 Oslo
1,000 m 2:11.96 WR 5 Septemba 1999 Rieti
1,500 m 3:28.12 11 Agosti 2000 Zürich
Maili 3:43.40 7 Julai 1999 Rome
2,000 m 4:50.08 30 Julai 1999 Stockholm
3,000 m 7:35.46 9 Juni 2000 Seville

Virejeleo hariri

Viungo vya nje hariri