Outkast au OutKast ni kundi la muziki wa hip hop lenye makazi yake huko mjini East Point, Georgia nchini Marekani. Kundi linaunganishwa na watu wawili, ambao ni André "André 3000" Benjamin na Antwan "Big Boi" Patton. Kundi lilianzishwa mnamo mwaka wa 1990. Awali walikuwa wakijulikana kama The OKB (The OutKast Brothers) lakini baadaye wakabadilisha jina la kundi na kuwa OutKast. Mtindo wa uimbaji wa zamani wa kundi hili ilikuwa mchanganyiko wa Dirty South na G-Funk.[1] Tangu hapo, lakini, funk, soul, electronic music, ushairi wa kutamka maneno, jazz, na elementi za blues zimekuwa zikiwekwa kwenye muziki wao.[2][3]

Outkast
Outkast kutoka 2001
Outkast kutoka 2001
Maelezo ya awali
Asili yake Atlanta na Savannah
Georgia, Marekani
Aina ya muziki Hip hop, Dirty South, G-Funk
Miaka ya kazi 1990-
Studio Laface Records
Ame/Wameshirikiana na Dungeon Family, Purple Ribbon All-Stars, T.I. Sleepy Brown, Goodie Mob, Witchdoctor, Organized Noize, UGK, Raekwon
Tovuti http://www.outkast.com
Wanachama wa sasa
Antwan "Big Boi" Patton
"André 3000" Benjamin

Wawili hawa ni moja kati ya makundi ya hip-hop yenye mafanikio kwa muda wote, kwa kupokea tuzo sita za Grammy Awards. Zaidi ya nakala milioni 25 zimeuzwa kwenye matoleo nane ya albamu za OutKast: albamu za studio sita, toleo la vibao vikali, na albamu ilioshinda tuzo ya Grammy Award-ikiwa kama (Albamu Bora) Speakerboxxx/The Love Below, albamu ya pamoja iliyojumlisha albamu moja-moja kutoka kwa kila mwanachama.

Diskografia hariri

Tazama pia Diskografia ya Outkast

Marejeo hariri

  1. allmusic Biography
  2. Erlewine, Stephen Thomas (2003). Speakerboxxx/The Love Below. Allmusic. Iliwekwa mnamo 2008-04-20.
  3. "OutKast propels hip-hop to new heights", CNN.com, 2004-04-15. Retrieved on 2008-04-19. 

Viungo vya Nje hariri

  Makala hii kuhusu mwanamuziki/wanamuziki fulani wa Marekani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Outkast kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.