Pamela Jelimo

Mkimbiaji wa mbio za kati wa Kenya

Pamela Jelimo (aliyezaliwa tarehe 5 Desemba 1989) ni mwanamichezo Mkenya anayebobea katika mita 800. Alishinda medali ya dhahabu kwenye Olimpiki ya mwaka wa 2008 mjini Beijing. Yeye ni mwanamke wa kwanza wa Kenya kushinda medali ya dhahabu ya Olimpiki na pia Mkenya wa kwanza kushinda Golden League Jackpot. Anashikilia rekodi ya dunia ya mita 800 ya wakiambiaji wachanga na rekodi ya Afrika ya wakimbiaji wazee wa umbali huo. Jelimo pia ni mmoja wa wanawake wachanga kuishindia Kenya medali ya dhahabu ya Olimpiki. Alishinda dhahabu hiyo ya mita 800 akiwa na umri wa miaka 18 tu.

Rekodi za medali

Pamela Jelimo
Women's Wanariadha
Anawakilisha nchi Bendera ya Kenya Kenya
Olympic Games
Dhahabu 2008 Beijing 800 m
African Championships
Dhahabu 2008 Addis Ababa 800 m
Fedha 2008 Addis Ababa 4x400 m relay

Maisha Yake ya Utotoni hariri

Pamela Jelimo alizaliwa katika kijiji cha Kiptamok, wilayani Nandi , katika mkoa wa Bonde la Ufa. [1] Mamake, Esther Cheptoo Keter, alikuwa mkimbiaji mzuri wa mita 200 na mita 400 lakini desturi za kikabila za Wanandi zilimaanisha kwamba kama binti ambaye ni kitinda mimba asingeweza kuolewa na ilimbidi awahudumie wazazi wake wenye umri wa makamo. Hata hivyo, alipewa ruhusa kuzaa watoto kwa wanaume tofauti, hivyo basi Jelimo alilelewa na mamake katika familia ya kaka watatu na dada wasita.[2] Jelimo alianza kukimbia mwaka wa 2003, akiwa na umri wa miaka 13, akiwa katika shule ya upili ya Koyo, divisheni Kaptumo, karibu na Kapsabet. [3] Alijifahamisha mwenyewe kama mwanamichezo aliyetimia kwa kushinda mashindao ya shule katika mita 100,mita 200 ,mita 400 , mita 800, mita 400 kutumia vikwazo na heptathlon. [4] Mwalimu wake wa michezo wa skuli ya upili, mwalimu Filipo N'Geno, alisema kwamba alikuwa akishindana na wavulana katika masafa mafupi kwani wasichana hawakumpa ushindani aliyohitaji.[2]

Familia yake ilikuwa maskini na ilijitahidi kulipa karo ya kumpeleka Jelimo katika shule ya upili - ndugu zake wawili wakubwa walikuwa tayari wameacha kusoma kwa hawakuweza kukidhi gharama. Yeye alikataa kuacha shule na alianza kuuza maziwa ya ng'ombe ya familia yake ili aweze kulipa karo.Alipitia miteremko kwa miguu iliaweze kuuza maziwa hayo katika soko la Chemase.[1] Mwalimu mkuu wa shule yao, Daniel Maru, alichangia fedha kwa ajili ya suti za maburuzo na viatu vya kukimbilia ili Jelimo aweze kuhudhuria kituo bora cha mbio cha masafa marefu nchini Kenya. Ilipotimia mwaka wa 2004, Jelimo alikuwa amefikia michuano ya mitaa ya mkoa katika mita 400.[3] Maru aliendelea na ukarimu wake. Alimruhusu Jelimo kuhitimu wakati bado alikuwa anadaiwa thamana ya mwaka mmoja ya karo. Hata hivyo, mamake alilazimishwa kuuza ng'ombe wake wa mwisho ndiposa Jelimo aweze kufanya mtihani wake.[2][4]

Manamo juni 2007, alimaliza wa tano katika mbio za mita 400 katika mashindano ya kitaifa ya Kenya kwa muda wa sekunde 55.82.[5] Aliendelea kujiboresha msimu wote. Alishinda medali ya dhahabu ya mita 400 katika mashindano ya Afrika ya wakimbiaji wachanga kwa kumaliza kwa muda wa sekunde 54.93 na kuweka rekodi ya kitaifa ya wakimbiaji wachanga ya Kenya katika mita 200 pamoja kwa sekunde 24.68. Jelimo alifurahishwa na mafanikio yake lakini kocha wake mpya, Zaid Kipkemboi Aziz, alipendekeza abadilishe na aanze kukimbia mita 800, kwa kusema kuwa atafanya bora katika mbio ya masafa marefu. Alianza kuifanyia kazi shurutisho la polisi la Kenya na alikuwa anafanya mazoezi na mwanariadha mkenya mwenzake Janeth Jepkosgei.

Jelimo alikimbia mbio yake ya kwanza ya mita 800 tarehe 19 Aprili 2008 katika majaribio ya Kenya ya michuano ya Afrika kwa muda wa dakika 2:01.02.[6] Lich ya masumbuko yake katika uanariadha wake, aliendelea kufanya kazi katika kituo cha Polisi cha Embu kama polisi na kupata shilingi 11000 kwa mwezi (kama euro 100).[7]

Kupanda Utukufu hariri

Utukufu wake ulianza katika mashindano ya ubingwa wa Afrika mwaka wa 2008 Athletics akiwa na umri wa miaka 18.[8] Muda wake, 1:58.70, ulikuwa rekodi mpya wa wanariadha wachanga. Tarehe 25 Mei 2008 alishinda mbio za mita 800 katika Grand Prix laHengelo na kuweka rekodi mpya ya wanariadha wachanga kwa muda wa dakika 1:55.76. Rekodi ya zamani (1:57.18) iliwekwa na Yuan Wang wa China mwaka wa 1993.[9] Ilikuwa pia rekodi mpya ya Kenya ambayo awali ilikuwa inashikiliwa na Janeth Jepkosgei (1:56.04 mwaka wa 2007).[10] Tarehe 1 Juni 2008 alikimbia mbio ya kuvutia ya mita 800 huko Berlin na alishinda ISTAF Golden League kwa muda wa dakika 1:54.99, rekodi mpya ya Afrika. Rekodi ya awali ya Afrika (1:55.19) iliwekwa na Maria Mutola mwaka wa 1994.

Tarehe 18 Julai mwaka wa 2008, aliboresha rekodi hiyo kwa kiasi kidogo tu kwa muda wa dakika 1:54.97 mjini Paris. Huu pia ulikuwa ushindi wake wa nne mfululizo katika AF Golden League, ambapo yeye alikuwa mmoja kati ya wawili tu waliyobaki kama wagombeaji wa jackpot ,mwingine akiwa mrukaji Blanka Vlašić. [11] Tarehe 18 Agosti 2008 Jelimo alishinda dhahabu katika mita 800 katika Olimpiki ya Beijing. Muda wake ulikuwa 1:54.87, kwa mara nyingine tena rekodi. Akawa mwanamke wa kwanza wa Kenya kushinda medali ya dhahabu ya Olimpiki.[12]

Aliendeleza rekodi yake ya kutoshindwa kwa kushinda pambano la Weltklasse Golden League mjini Zürich tarehe 29 Agosti 2008 na kuboresha wakati wake wa kibinafsi hadi dakika 1:54.01.[13] Huu ulikuwa utendaji wa tatu wa kasi zaidi milele, nyuma ya Nadezhda Olizarenko na rekodi ya dunia ya Jarmila Kratochvílová. Katika mashindano ya ukumbusho wa Van Damme mjini Brussles, fainali ya AF Golden League, Jelimo alishinda mbio za mita 800 kwa muda wa 1:55.16.[14] Kama mwanariadha wa kipekee kushinda tukio moja (mbio ya mita 800) katika mikutano yote 6 ya Golden League, yeye alishinda shindano la jackpot la dola milioni 1. Mwanariadha yule mwingine aliyekuwa amebaki katika shindano hilo, Blanca Vlasic, alishindwa kushinda tukio la mwisho.[15] Yeye ni Mkenya wa kwanza kushinda Golden League jackpot.[16]

Alilikunja jamvi msimu wake wa kutoshindwa kwa kushinda mbio yake (mita 800) katika fainali ya IAAF World Athletics wa mwaka wa 2008. Baada ya tukio hilo alirejea Kenya kwa mara ya kwanza tangu majaribio ya Olimpiki na kukaribishwa na sikukuu nyingi. Tarehe 18 Septemba 2008 katika mji wa Kapsabet, njia - njia ya Pamela Jelimo (Pamela Jelimo Street)- ilitajwa kwa heshima yake.[17]

Jelimo aliorodheshwa katika jamii ya wanariadha wanawake bora mwaka huo na IAAF pamoja na Yelena Isinbayeva na Tirunesh Dibaba, lakini Isinbayeva alilishinda tuzo hilo. Hata hivyo, Jelimo alituzwa tuzo la Ufunuo wa mwaka wa IAAF (IAAF Revelation of the year Award) na tuzo la mwanamichezo mwanamke wa mwaka wa Kenya. [18][19]

Alikosa msimu wa ndani (indoor) wa 2009 kutokana na kunyooka kwa achilles wakati wa mazoezi.[20] Badala yake, alianza msimu wake mwezi wa Aprili katika pambano la Athletics Kenya huko Kakamega, na kukimbia mbio za mita 200 na 1,500 kwa ajili ya mazoezi.[21] Tarehe 23 Mei alikimbia mbio yake ya kwanza ya mita 800 ya mwaka wakati wa pambano la Kimataifa wa Mohammed wa VI mjini Rabat, Morocco, na kumaliza wa sita (muda wa 2:02.46) - hii ilikuwa mbio ya kwanza ya mita 800 ambayo hakushinda.[22] l Wiki mbili baadaye alimaliza wa mwaisho katika pambano la Prefontaine Classic huko Eugene, Oregon. [23] Kutokana na matokeo haya mabaya, alijinuiza kwa mazoezi kwa zaidi ya mwezi. Alifanikiwa kurejea mbioni kwa kushinda pambano la Heusden-Zolder tarehe 18 Julai kwa kukimbia chini ya dakika mbili (1:59.59).[24][25]

Alishindana katika mashindano ya dunia ya mwaka wa 2009 lakini hakumaliza nusu fainali yake.[26]

Maisha ya Kibinafsi hariri

Jelimo aliolewa na Petro Kiprotich Murrey, ambaye pia ni mkimbiaji wa mita 800, mwishoni mwa 2007. Hawakuwa na waya wa harusi kubwa;uwezo wao haukuwawezesha na badala yake walikuwa na sherehe ndogo. Ndoa haikufichuliwa kwa hadhara hadi Desemba 2008.[27].

Majilio hariri

Ubora wa kibinafsi hariri

Tarehe Tukio Ukumbi Muda
Julai 2007 mita 200 Ouagadougou, Burkina Faso sekunde 24.68
26 Juni 2008 mita 400 Nairobi, Kenya sekunde 52.78
29 Agosti 2008 mita 800 Zürich, Uswisi dakika 1:54.01
17 Aprili 2009 mita 1500 Kakamega, Kenya dakika 4:19.31

Sahihi tangu 10 Oktoba 2008. Habari yote imetoka IAAF.

Rekodi ya mashindano hariri

mwaka Michuano Ukumbi Matokeo Ziada
2007 African Junior Championships Ougadougou, Burkina Faso 3 mita 200 [28]
1 mita 400
2008 African Championships Addis Ababa, Ethiopia 1 mita 800
2 mita 4x400
Michezo ya Olimpiki Beijing, Uchina 1 mita 800
World Athletics Final Stuttgart, Ujerumani 1 mita 800

Marejeleo hariri

  1. 1.0 1.1 Bartoo, Vincent (7 Septemba 2008). Grand reception awaits superstar Jelimo. The Standard. Iliwekwa mnamo 8 Oktoba 2008.[dead link]
  2. 2.0 2.1 2.2 Rice, Xan (4 Oktoba 2008). Bittersweet return for Olympic star. The Guardian. Iliwekwa mnamo 8 Oktoba 2008.
  3. 3.0 3.1 Brown, Matthew (19 Agosti 2008). Jelimo - really starting something. IAAF. Iliwekwa mnamo 8 Oktoba 2008.
  4. 4.0 4.1 Oyoo, Jack (30 Septemba 2008). Village celebrates Jelimo's success. Reuters. Iliwekwa mnamo 8 Oktoba 2008.
  5. Results June 2007. Africathle.com (16 Juni 2007). Iliwekwa mnamo 8 Oktoba 2008.
  6. Ramsak, Bob (1 Juni 2008). Berlin witnesses Jelimo, 800m revelation - ÅF Golden League. IAAF. Iliwekwa mnamo 8 Oktoba 2008.
  7. Okoth, Omulo (22 Septemba 2008). Top athletes’ affinity with armed forces. The Standard. Jalada kutoka ya awali juu ya 2008-09-24. Iliwekwa mnamo 8 Oktoba 2008.
  8. [29] ^ Powell, David (4 Mei 2008) Chelimo defeats Mutola, K. Bekele takes 5000m - African Championships, final day IAAF Retrieved on 14 Desemba 2008
  9. [30] ^ Ramsak, Bob (24 Mei 2008) Saladino, Jelimo and Gebrselassie the stars in Hengelo – IAAF World Athletics Tour IAAF Retrieved on 14 Desemba 2008
  10. [31] ^ Jelimo sets new world junior record Daily Nation(26 Mei 2008) Retrieved on 14 Desemba 2008
  11. [32] ^ Turner, Chris (18 Julai 2008) Jelimo 1:54.97; Robles 12.88; Wariner 43.86 in Paris - ÅF Golden League, Paris IAAF Retrieved on 14 Desemba 2008
  12. [33]^ Okoth, Omulo (18 Agosti 2008) Kenya wins two Olympic gold medals The Standard Retrieved on 14 Desemba 2008
  13. [34] ^ Weltklasse 2008 results Weltklasse Retrieved on 14 Desemba 2008
  14. Memorial Van Damme 2008. IAAF (5 Septemba 2008). Jalada kutoka ya awali juu ya 2010-01-21. Iliwekwa mnamo 7 Septemba 2008.
  15. Jelimo wins Golden League jackpot. International Herald Tribune (5 Septemba 2008). Jalada kutoka ya awali juu ya 2008-09-19. Iliwekwa mnamo 7 Septemba 2008.
  16. [39] ^ Kenya's heroine Jelimo spurs stampede at home arrival AFP (16 Septemba 2008) Retrieved on 14 Desemba 2008
  17. [40] ^ Ng'Etich, Peter (18 Septemba 2008) Pomp as street is named after million dollar girl Daily Nation Retrieved on 14 Desemba 2008
  18. [41] ^ Makori, Elias (23 Novemba 2008) Bolt and Isinbayeva named top athletes for '08 Daily Nation Retrieved on 14 Desemba 2008
  19. [42] ^ Kamuzo Banda, Tim (23 Januari 2009) Moment of glory for Wanjiru and Jelimo The Daily Nation Retrieved on 23 Februari 2009
  20. [43] ^ Mutwiri, Mutuota (18 Februari 2009)Jelimo cancels trips to indoor meetings The Standard Retrieved on 23 Februari 2009
  21. [44] ^ IAAF, 19 Aprili 2009: Cheruiyot and Jelimo spice-up Kakamega track meet Retrieved on 20 Aprili 2009
  22. [45] ^ Athletics Weekly, 23 Mei 2009: Meadows stuns Jelimo in Rabat
  23. [46]^ The Standard, 9 Juni 2009: Olympic medallist Kiprop tops Oregon meeting
  24. [47] ^ NACHT VAN DE ATLETIEK: 800m Women ; Official result
  25. [48] ^ Hendrix, Ivo (19 Julai 2009) Jelimo returns with 1:59.59 in Heusden-Zolder IAAF Retrieved on 22 Julai 2009
  26. [49]^ 2009 IAAF World Championships - 800 metres women semi-final results
  27. [50] ^ Mutuota, Mutwiri (12 Desemba 2008) Marital bliss for million-dollar girl The Standard Retrieved on 14 Desemba 2008
  28. DUNIANI Junior Athletics HISTORIA ( "WJAH") Junior Mabingwa wa Afrika 2007 Archived 7 Aprili 2014 at the Wayback Machine.

Viungo vya nje hariri