Papa Urban I alikuwa Papa kuanzia tarehe 14 Oktoba 222 hadi kifo chake tarehe 23 Mei 230[1]. Alitokea Roma, Italia.

Papa Urbano I

Alimfuata Papa Kalisto I akafuatwa na Papa Ponsyano.

Urban I ni Papa wa kwanza ambaye tarehe zake zina hakika ya kihistoria[2]. Inaonekana hakukuwa na dhuluma za serikali wakati wa Upapa wake, lakini alipaswa bado kupambana na farakano la Hipoliti wa Roma[3] pamoja na kuongoza kwa uaminifu Kanisa la Roma miaka minane.

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu, hasa tarehe 19 Mei, sikukuu yake[4].

Tazama pia hariri

Maandishi yake hariri

Tanbihi hariri

  1. https://www.vatican.va/content/vatican/en/holy-father.index.html#holy-father
  2. Kung, Hans. The Catholic Church: A Short History. New York; The Modern Library, 2003, p. 41
  3. "Pope Urban I". Catholic Encyclopedia. New York: Robert Appleton Company. 1913. http://www.newadvent.org/cathen/15209a.htm.
  4. Martyrologium Romanum: ex Decreto Sacrosancti oecumenici Concilii Vaticani II instauratum auctoritate Ioannis Pauli P.P. II promulgatum, Romae 2001, ISBN 8820972107

Viungo vya nje hariri

  Makala hii kuhusu Papa fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Papa Urban I kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.