Paroko ni padri aliyekabidhiwa na Askofu uchungaji wa parokia, ambayo ni sehemu ya jimbo.

Paroko wa Campora San Giovanni, Apollinaris Mashughuli Massawe kutoka Tanzania.

Jina hilo linatokana na Kigiriki cha zamani πάροικος (pàroikos), ambapo asili ni kitenzi παρà οἰκεω (parà oikéo), yaani "kuishi jirani", "kuishi kandokando", kulingana na Askofu aliyeishi mbali, katika Kanisa kuu.

Katika Kanisa Katoliki la Kilatini huduma ya maparoko inaratibiwa na Mkusanyo wa Sheria za Kanisa katika kanuni 519-534.

Makala hii kuhusu dini ya Ukristo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Paroko kama historia yake, matokeo au athari zake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.