Remakli (pia: Remacle, Remaclus, Remaculus, Rimagilus; Aquitaine, leo nchini Ufaransa, karne ya 6 mwishoni au karne ya 7 mwanzoni – Stavelot, leo nchini Ubelgiji, 673 hivi) alikuwa mmonaki padri huko Luxeuil aliyetumwa kuwa abati wa kwanza [1] wa monasteri ya Solignac [2] halafu akakabidhiwa nyingine tatu [3].

Sanamu yake huko Stavelot.

Mwaka 650[4] alichaguliwa kuwa askofu wa Maastricht[5]. Hapo kwa miaka kumi na miwili alijitahidi kufanya wakazi Wapagani wa Flandria waongokee Ukristo halafu akarudi monasterini [6][7].

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 3 Septemba[8].

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

Marejeo hariri

  Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.