Rio de Janeiro ni jiji kubwa la pili nchini Brazil baada ya São Paulo.

Sanamu ya Mwokozi.
Rio kutoka angani.
Favela-mtaa wa mabanda.

Ilikuwa mji mkuu wa nchi hadi tarehe 21 Aprili 1960. Leo ni mji mkuu wa jimbo la shirikisho la Rio de Janeiro. Mwaka 2000 rundiko la jiji lilikuwa na wakazi 5,473,909.

Rio de Janeiro ni jiji la Brazil linalojulikana zaidi kote duniani. Ni kitovu cha utalii na cha utamaduni. Kanivali yake inavuta wageni wengi kila mwaka. Mlima wa Corcovado unabeba Sanamu ya Mwokozi ambayo ni sanamu kubwa ya Yesu yenye kimo cha mita 30.

Viungo vya nje hariri

  Makala hii kuhusu maeneo ya Brazil bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Rio de Janeiro kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.