Riwaya (kutoka neno la Kiarabu رواية riwaya ) ni kazi andishi ya fasihi ambayo kwa kawaida ni ndefu kuliko hadithi fupi. Urefu wa riwaya, maana yake ni kwamba msuko simulizi umejengeka vizuri, kuna wahusika wengi, unaenea muda mrefu, na mada zake ni nzito na pana kiasi.

Riwaya ya Adolphe

Mifano mizuri ya riwaya kwa lugha ya Kiswahili ni Nagona au Mzingile, zilizoandikwa na mwandishi Euphrase Kezilahabi.

Kamusi ya Fasihi iliyotolewa na K. W. Wamitila inataja aina nyingi tofauti za riwaya, k.m. riwaya sahili, riwaya changamano, riwaya kiambo, riwaya ya kibarua na nyingine nyingi.

Utunzi au uandishi wa riwaya hariri

Uhariri wa riwaya hariri

Marejeo hariri

  • Wamitila, Kyallo Wadi (2003), Kamusi ya Fasihi - Istilahi na Nadharia, Nairobi: Focus Publications. ISBN 9966-882-79-6
  • Samwel, Method, Selemani Amina na Akech Kabiero (2013), "Ushairi wa Kiswahili: Nadharia, Mifano na Mwongozo kwa Walimu wa Kiswahili," Dar es Salaam: MEVELI Publishers. ISBN: 978-9987-9735-0-7
  Makala hii kuhusu mambo ya fasihi bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Riwaya kama historia yake, uenezi au maendeleo yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.