Robert Napunyi Wangila (alizaliwa mnamo 3 Septemba 1967 katika mji mkuu wa Nairobi - na alifariki mnamo 24 Julai 1994) alikuwa bondia wa Kenya wa uzito wa "welterweight" ambaye alishinda medali ya dhahabu katika Michezo ya Olimpiki ya mwaka wa 1988. Yeye bado ndiye mwanaspoti wa Kenya aliyeshinda medali ya dhahabu ya Olimpiki ambayo si ya riadha.

Rekodi za medali
Ubondia wa Wanaume
Anawakilisha nchi Bendera ya Kenya Kenya
Michezo ya Olimpiki
Dhahabu 1988 Seoul Welterweight
Michezo ya All-Africa
Dhahabu 1987 Nairobi Featherweight

Matokeo ya Olimpiki hariri

  • Raundi ya Kwanza
  • Alimshinda Đorđe Petronijević (Yugoslavia) RSC 2
  • Alimshinda Khaidan Gantulga (Mongolia) TKO 2
  • Alimshinda Hristo Furnigov (Bulgaria) 5-0
  • Alimshinda Jan Dydak (Poland) ambaye hakutokea kwa pigano
  • Alimshinda Laurent Boudouani (Ufaransa) KO 2

Wasifu wa baadaye hariri

Robert Wangila aligeuka kuwa bondia wa utaalamu mwaka wa 1989 na kwa ujumla alikuwa na rekodi ya 22-5-0.

Kifo chake hariri

Wangila alikufa kutokana na majeraha aliyopata mwaka 1994 wakati alikuwa anapambana na David Gonzales katika mji mkuu wa Las Vegas. Wangila alikuwa amepigwa vibaya sana na alikuwa kwa hali mbaya kana kwamba refaro Joe Cortez alisimamisha mechi na kumpa Gonzales ushindi, licha ya Wangila kupinga sana. Baada ya mechi, Wangila alipoteza fahamu na kuzirai katika chumba chake cha kubadilisha. Hatimaye alitangazwa amekufa baada ya masaa thelathini na sita.

Wangila alikuwa amegeuka kutoka kuwa Mkristo na kuwa Mwislamu wakati alipokuwa bado Marekani, na kwa hiari liliomba kwamba yeye azikwe kulingana na matakwa ya mke wake wa Kiislamu. Hii ilikuwa changamoto kwa familia ya Wangila nchini Kenya, lakini mwamuzi alitangaza kwa neema ya mazishi Waislamu kuzikwa.

Marejeo hariri

Viungo vya nje hariri

  Makala hii kuhusu mtu huyo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Robert Wangila kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.