Ruiru ni mji wa Kaunti ya Kiambu, ipatikanayo katikati ya Kenya.

Ruiru
Nchi Kenya
Kaunti Kiambu
Idadi ya wakazi
 - Wakazi kwa ujumla 238,858
Mji wa Ruiru.

Jiografia hariri

Mji huu uko katika umbali wa takribani kilomita 3 kutoka katika Mpaka wa Nairobi.

Una eneo la km2 292 na umezungukwa na mashamba ya Kahawa. Ruiru ni mmoja kati ya miji inayotambulika zaidi nchini Kenya, ambao unaweza kufikika kwa urahisi kupitia barabara au reli.

Idadi ya Wakazi hariri

Mji huu umekuwa na ongezeko la idadi ya watu, kutokana na uhaba wa nyumba mjini Nairobi.

Mwaka 2009 ulikuwa na wakazi 238,858[1].

Hata hivyo, mji huu umeng'ang'ana kuwatosheleza wakazi wake.

Uchumi hariri

 
Moja ya majengo ya Ruiru.

Wengi wa wakazi wa Ruiru ni wafanyabiashara wenye asili ya Kikuyu.

Mji huu pia una matawi ya benki kadhaa kama vile Benki ya Equity, Benki ya Family, Benki ya Cooperative na Benki ya Barclays.

Pia kuna viwanda mbalimbali katika mji huo.

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

  1. Sensa ya Kenya 2009 Archived 9 Januari 2019 at the Wayback Machine., tovuti ya KNBS, ilitazamwa Januari 2009.

Viungo vya nje hariri

Coordinates: 1°08′56″S 36°57′25″E / 1.14889°S 36.95694°E / -1.14889; 36.95694