Sibel Kolcak

Mwanasoka

Sibel Kolçak (alizaliwa 3 Januari, 1990) ni mwamuzi wa mpira wa miguu wa Uturuki aliyeorodheshwa kwenye orodha ya waamuzi wa wanawake wa FIFA . Pia ni mwalimu na anaishi Zonguldak, Uturuki.[1][2]

Maisha ya awali hariri

Sibel Kolçak alizaliwa huko Zonguldak, Uturuki. Alisomea masuala ya Utawala wa michezo katika Chuo Kikuu cha Sakarya, na akarejea baada ya kuhitimu katika mji aliozaliwa wa Zonguldak .

Kazi ya uamuzi hariri

Alianza kazi yake ya uamuzi mnamo 2007 katika mji aliozaliwa, na alichezesha rasmi kama mwamuzi msaidizi kwa mara ya kwanza mnamo 1 Machi 2008.

Alichezesha mechi yake ya kwanza katika nafasi ya mwamuzi mnamo Novemba 7, 2009, kwenye mechi ya Ligi ya Coca-Cola Academy chini ya miaka 14.

Aliteuliwa kuwa mwamuzi katika Ligi ya wanaume ya A2 League na Women's Second League, na hatimaye Desemba 22, 2013, alipandishwa hadhi na kuchezesha mechi ya Ligi ya daraja la kwanza ya Wanawake.[3]

Marejeo hariri

  1. "SİBEL KOLÇAK - Hakem Bilgileri TFF". www.tff.org. Iliwekwa mnamo 2023-04-14. 
  2. "'Koşamayan' hakem maç yönetti!". www.hurriyet.com.tr (kwa Kituruki). Iliwekwa mnamo 2023-04-14. 
  3. "SİBEL KOLÇAK - Hakem Bilgileri TFF". www.tff.org. Iliwekwa mnamo 2023-04-14. 
  Makala hii kuhusu mtu huyo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Sibel Kolcak kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.