Turibio wa Mongrovejo

Turibio wa Mongrovejo (16 Novemba 153823 Machi 1606) alikuwa askofu wa Kanisa Katoliki nchini Peru.

Mtakatifu Toribio Alfonso de Mogrovejo.

Alitangazwa mwenye heri na Papa Inosenti XI tarehe 2 Julai 1679 halafu mtakatifu na Papa Benedikto XIII tarehe 10 Desemba 1726.

Tarehe ya kifo chake, yaani 23 Machi ndiyo sikukuu yake[1].

Maisha hariri

Turibio wa Mongrovejo alizaliwa nchini Hispania mnamo mwaka 1538.

Alijifunza sheria huko Salamanca, na mwaka 1580, akiwa bado mlei, aliteuliwa kuwa Askofu wa Lima nchini Peru, akaenda Amerika.

Alikuwa motomoto kwa kazi za kitume, akiitisha mikutano mbalimbali ili kurekebisha mambo ya dini na maadili na kukomesha makwazo ya waklero katika nchi nzima.

Kwa nguvu zote alitetea haki za Kanisa, mara kadhaa alitembelea, hasa kwa miguu, Wakristo wa jimbo lake pana, na kufanya kazi kwa muda mrefu kwa mafaa ya wenyeji wa Peru.

Alifariki dunia mwaka 1606.

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

Viungo vya nje hariri

  Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.