Ulaya ya Magharibi

Ulaya ya Magharibi ni sehemu ya magharibi ya bara la Ulaya. Kuna maelezo tofauti ni nchi zipi ambazo ni sehemu ya kanda hilo. Maelezo hutofautiana kutokana na njia mbalimbali za kuangalia sehemu hiyo: kwa maana ya kijiografia, kihistoria, kisiasa au kiutamaduni.

Ulaya ya Magharibi kijiografia kufuatana na CIA-Factbook (njano); njano nyeupe: Ulaya ya Kusini-Magharibi

Kanda la kijiografia hariri

Kama kanda la kijiografia mara nyingi nchi zifuatazo zinahesabiwa kuwa Ulaya ya Magharibi:

 
Ulaya ya Magharibi kufuatana na mpangilio wa Umoja wa Mataifa (buluu nyeupe);
Buluu nyeusi: Ulaya ya Kaskazini
Kijani: Ulaya ya Kusini
Nyekundu: Ulaya ya Mashariki

Mpangilio wa Umoja wa Mataifa hariri

Umoja wa Mataifa umepanga kanda hili tofauti, hasa kwa kuhesabu Ufalme wa Muungano upande wa Ulaya ya Kaskazini, lakini pia kwa kuingiza Ujerumani, Austria na Uswisi ambazo zinahesabiwa mara nyingi kama sehemu ya Ulaya ya Kati wakati mpangilio wa UM hauna Ulaya ya Kati.

 
Ulaya ya Magharibi kisiasa wakati wa Vita Baridi
Buluu: Ulaya ya Magharibi (NATO)
Kijivu: Nchi zisizofungamana na upande wowote
Nyekundu: Ulaya ya Mashariki (upande wa Umoja wa Kisovyeti)

Ulaya ya Magharibi kihistoria katika karne ya 20 hariri

Wakati wa "vita baridi" Ulaya ya Magharibi ilimaanisha mara nyingi nchi zote za Ulaya zilizofungamana na upande wa magharibi yaani Marekani na NATO dhidi nchi za kikomunisti zilizoshikamana na Umoja wa Kisovyeti.