Wamambwe ni kabila la watu wanaoishi Tanzania katika Mkoa wa Rukwa, Wilaya ya Sumbawanga. Wako pia upande wa Zambia, huku asili ya kabila ni Zambia, hasa eneo karibu na mji wa Mbala.

Lugha yao ni Kimambwe. Wamambwe na Warungu wanaongea lugha moja yenye lahaja mbili. Ukisikia wanaongea utafikiri Kifipa lakini maneno yao mengi wanapenda kuyachanganya na Kiingereza.

Ni kabila ambalo kwa kuongea wanafanana na Walungu utofauti wao upo kwa mambo madogo madogo kama vile ngoma za asili, adabu, usafi, ukali na haraka ya kuongea. Asili ya Wamambwe ni upole wakati Mlungu hataki mchezo, ila Mmambwe akichukia anachukia kwelikweli.

Ni wakulima wa maharage, mahindi, ulezi, mhogo, viazi na mboga za majani. Vile kamaa jamii nyingine za Kibantu ni wafugaji na wawindaji wadogo. Wanapenda kula ugali kwa maharage na mlenda uitwao mpondesha, yaani mlenda mzito.

Koo zao kwa upande wa wanaume mara nyingi huanzia na "Si": kwa mfano Sinyagwe, Sichula, Siame, Sikonda, Simfukwe, Sichone, Simuyemba, Simpokolwe, Simte, Sikaumbwe, Simchile, Simpanzye, Sikalumba.

Kwa upande wa wanawake huanzia kwa "Na": kwa mfano Nanyangwe, Nachula, Namfukwe, Nayame, Nakonda, Nachone, Namuyemba, Nampokolwe, Namte, Nakaumbwe, Nnampanzye, Nakalumba n.k.

Kumbe Wafipa asili hawana majina hayo, ila wenyewe utasikia Nandi, Kapufi, Kipesha, Chula, Ngua, Nyami na mengineyo.

Ukoo mkubwa wa kichifu kwa upande wa Wamambwe ni akina Sichula kama vile Kutazungwa, Mfwambo, Mwamba, Sokoro n.k. wakati kwa Walungu ni akina Sikazwe na Sichilima kama vile Tafuna, Kapembwa, Zombe, Londe n.k.

Halafu tabia yao, mtoto mdogo anapomwita mtu mkubwa kuonyesha heshima lazima amwite kwa wingi, yaani mtu mmoja anaitwa kama watu wengi; mfano baba kwa Kimambwe huitwa tata, lakini kiheshima ataitwa YATATA, mama huitwa mayo, kiheshima YAMAYO.

Vile Wamambwe ni wafanyabiashara ya mazao ya mahindi na maharage. Ukiangalia kwa upande wa Wamabwe walioko Zambia wamepiga hatua kutokana na miundombinu waliyojengewa na taifa lao, ndio hata wale waliosoma sana wanapatikana ile nchi. Tatizo linalosumbua kwa upande wa Tanzania ni miundombinu mibovu kiasi kwamba jamii hii inaonekana kama haipo Tanzania, ndio maana watu wengi huona kama kabila geni nchini.Kwanza nashukru kwa makala hii nzuri,kipengele cha machifu Wawamambwe, machifu wa Kabila la wamambwe ni wakina Sichula na wakina Simfukwe mfano upande wa Zambia Chifu Nsokolo ni Sichula upande wa Zambia, wakati Chifu Kutazungwa ni Sichula Chifu Umambwe upande wa Tanzania,Mwamba ni Simfukwe Chifu upande wa Umambwe Zambia na Mulamba ni Simfukwe Chifu Upande wa Tanzania.Majina haya kichifu ni ya kiutawala mala nyingine yanabadilika kulingana na jina atakaloamua kulitumia mtawala mpya.

Makala hii kuhusu utamaduni wa Tanzania bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Wamambwe kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.