Wateatini (kwa Kiingereza jina kamili la shirika ni: Congregation of Clerks Regular of the Divine Providence, kifupi: "C.R.") ni utawa wa kikleri wa Kanisa Katoliki ulioanzishwa na Gaetano wa Thiene, Paolo Consiglieri, Bonifacio da Colle, na Giovanni Pietro Carafa (ambaye akawa Papa Paulo IV).

Kanisa la Wateatini mjini Roma, Sant'Andrea della Valle.

Aina hiyo mpya ya shirika likawa kielelezo kwa mengine mengi, kama vile Wajesuiti, Wabarnaba, Wasomaski n. k.

Lengo kuu la shirika hilo lilikuwa kurudisha wenye daraja takatifu kwenye uadilifu. Gaetano wa Thiene aliwaachia wanafunzi wake hasa jukumu la kufuata mtindo wa maisha ya Mitume wa Yesu.

Kati ya watakatifu wa shirika hilo, mbali ya mwanzilishi, wapo Andrea Avellino, Yosefu Maria Tomasi. Wapo pia wenye heri kadhaa.

Kadiri ya Annuario Pontificio, tarehe 31 Desemba 2014 Wateatini duniani walikuwa 170 katika nyumba 34. Kati yao 139 walikuwa mapadri.

Makala hii kuhusu Kanisa Katoliki bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Wateatini kama historia yake au maelezo zaidi?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.