Wilaya ya Laikipia


Wilaya ya Laikipia ilikuwa moja kati ya wilaya sabini na moja za Jamhuri ya Kenya hadi ilipopitishwa katiba mpya ya nchi (2010).

Wilaya ya Laikipia
Mahali paWilaya ya Laikipia
Mahali paWilaya ya Laikipia
Mahali pa Wilaya ya Laikipia katika Kenya
Nchi Bendera ya Kenya Kenya
Mji mkuu Nanyuki
Eneo
 - Jumla 8,696.1 km²
Idadi ya wakazi (2009 Sensa[1])
 - Wakazi kwa ujumla 399,227

Ilikuwa wilaya mojawapo ya Mkoa wa Bonde la Ufa iliyoko kwenye Ikweta.

Makao makuu yalikuwa mjini Nanyuki.

Kwa sasa imekuwa kaunti ya Laikipia.

Wilaya hii ilikuwa na vituo viwili vikuu vya soko: Nanyuki kwenye upande wa kusini mashariki, na Nyahururu kwenye upande wa kusini magharibi.

Wakikuyu walikuwa takribani 60% ya idadi ya watu wote kwenye wilaya hii, huku idadi iliyosalia ikijumuisha watu wa makabila mengine, ni pamoja na Mukogodo Masai, Wasamburu, Wameru, Waborana, Wakalenjin, Wasomali, Wazungu, Watu wa asili ya Asia, na Waturkana, wakiipa wilaya hii idadi ya watu tofauti tofauti. Mashamba mengi yanamilikiwa na idadi ndogo ya masetla wa ukoloni.

Shughuli kuu za kiuchumi katika wilaya hii ni utalii na kilimo, haswa mimea za mbegu, ufugaji na kilimo cha maua,matunda na mboga.

Hali ya hewa ya wilaya hii ni ya baridi kiasi, ikiwa na msimu wa mvua na kiangazi.

Serikali za Mtaa (Mabaraza)
Baraza Aina Idadi ya Watu* Wakaazi wa mjini*
Nanyuki Manispaa 39,838 31,577
Nyahururu Manispaa 32,120 24,751
Rumuruti Mji 31,649 4,249
Laikipia Kaunti 218,580 3,610
Jumla - 322,187 64,187
* 1999 census. Source: [1]
Maeneo ya utawala
Tarafa Idadi ya Watu* Wakaazi wa mjini* Makao makuu
Mkoa wa Kati 77,478 28,489 Nanyuki
Lamuria 38,517 0 Lamuria
Mukogondo 13,176 624
Ngarua 65,545 2,813 Kinamba
Nyahururu 37,412 22,459 Nyahururu
Olmoran 11,069 0
Rumuruti 78,894 4,061 Rumuruti
Jumla 322,187 58,466 -
* 1999 census. Sources: [2], [3],

Wilaya hii ina Majimbo ya Uchaguzi mawili:

Marejeo hariri

Viungo vya nje hariri