Yeha ni kijiji kilichopo upande wa kaskazini mwa nchi ya Ethiopia. Kipo katika eneo la Mehakelegnaw katika mkoa wa Tigray.

Jengo lililokuwa kubwa la Yeha katika mkoa wa Tigay, nchini Ethiopia.

Sayansi ya ujenzi hariri

Jengo refu kuliko yote nchni Ethiopia lipo katika eneo la Yeha. Huitwa pia Hekaru Kubwa la Yeha. Hili ni jengo refu lililojengwa katika staili ya Sabean na limejengwa karibu na wakati yalipojengwa baadhi ya majengo yalipo Arabia ya Kusini. Katika kipindi cha miaka ya 700 kabla ya Kristo. Japokuwa kifaa cha kutambua umri wa vitu vya kale kimefanyika katika baadhi ya vitu katika eneo la Yeha, lakini tarehe hii inatolewa na maandishi ya eneo hilo .[1]. David Phillipson anasema kuwa, ujenzi huu wenye uzuri wa kuvutia, umedumu kwa muda wote huo kutokana na utunzaji kutoka kwa wajenzi wake, wanaokadiwa kuanza kujenga katika karne ya sita baada ya Kifo cha Yesu, kwa kutumia kalenda ya kanisa "[1] Maeneo mengine ya kihistoria katika eneo la Yeha ni pamoja na Grat Beal Gebri, sehemu iliyoharibwa na portico yenye ukubwa a mita 10 kwa upana napia kuna sehemu ya makaburi ya iliyo na mawe mengi na mengi yakiwa yapo chini ya ardhi iliyogundulika mwaka 1960.Moja kati ya ushahidi unaonesha kuwa moja ya mawe yana makaburi ya kifalme, wakti jingine, linaaminika kuwa watu wa kale walikuwa wakiishi kiasi cha kilometa moja kutoka upande wa kusini ili Yeha ya sasa.[2]

Yeha ipia ni sehemu inayopatikana kanisa kubwa zaidi la nchini Ethiopia,ambalo kwa mujibu wa taratibu za kiutamaduni lilianzishwa na Abba Aftse, moja kati ya wale watakatifu tisa. Kwa mujibu wake, Francisco Álvares alieleza wakati alipotembelea mji huu mwaka 1520, ambapo aliuita "Abbafaçem" ambapo alielezea jinsi ya makanisa hayo yalivyokuwa [3] Alieleza kuwa kanisa hili ni imara na kuwa lisingeweza kuharibika katika siku ya hivi karibuni, kama ambavyo Deutsche Aksum-Expedition alielezea katika miaka ya kwanza ya karne ya 20 (Jengo la sasa ambalo linatangaza Mji wa Aksumitna kuwa na michoro mbalimbali ya eneo hilo, lilijengwa kati ya mwaka 1948 na 1948.[4]

Yeha pia limekuwa ni eneo la kufanyia tafiti mbalimbali za Kihandisi, tangu mwaka 1952, na Taasisi ya Uhandisi ya Ethiopio.Ethiopian Institute of Archeology. Japokuwa hii iliingiliwa katika uongozi wa Derg lakini hali ilirudi kama awali tena mwaka 1993, na kuzinduliwa na wafanyakazi kutoka Ufaransa.

Marejeo hariri

  1. 1.0 1.1 David W. Phillipson, Ancient Churches of Ethiopia (New Haven: Yale University Press, 2009), p. 36
  2. Phillipson, Ancient Churches, pp. 32, 37
  3. Francisco Alvarez, The Prester John of the Indies translated by C. F. Beckingham and G. W. B. Huntingford (Cambridge: Hakluyt Society, 1961), pp. 140f
  4. Phillipson, Ancient Churches, p. 37

Viungo vya Nje hariri