Yui Hasegawa (alizaliwa 29 Januari 1997) ni mchezaji wa mpira wa miguu nchini Japani ambae anacheza kama kiungo wa timu ya taifa ya Japani pamoja na klabu ya Manchester City inayoshiriki ligi ya Wanawake ya Super League.

Alizaliwa huko Sendai, Mkoa wa Miyagi na kukulia Toda, Saitama. Hasegawa alicheza mpira na timu ya vijana ya Tokyo Verdy Beleza kabla ya kuanza kucheza na timu kubwa mnamo mwaka 2013. Mwaka 2021 Hasegawa alijiunga na AC Milan kabla ya kuhamia West Ham United mwishoni mwa msimu wa 2020-21 wa ligi ya Serie A. Alijiunga na Manchester City katika majira ya joto mwaka 2022 baada ya kucheza msimu mmoja na timu ya West Ham United. [1][2][3]

Marejeo hariri

  Makala hii kuhusu mchezaji mpira fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Yui Hasegawa kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.