Aaron Mokoena

Mchezaji mpira wa Afrika Kusini

Aaron Tebomo Mokoena (amezaliwa Johannesburg, 25 Novemba 1980) alikuwa mwanakandanda wa kulipwa kutoka nchi ya Afrika Kusini aliyecheza kama kiungo wa kati.

Aaron Mokoena

Wasifu wa Klabu hariri

Alihamia klabu ya Bundesliga ya Bayer Leverkusen kisha akahamia Ajax iliyoko Uholanzi, kabla ya kukopwa nje kwa klabu ya Germinal Beerschot, na tena akajipata kama nahodha wa kikosi.

Mokoena alihamia klabu ya Blackburn na aliichezea klabu hiyo mechi yake ya kwanza mnamo 8 Januari 2005, dhidi ya Cardiff City katika Kombe la FA kama dakika 43 kama mbadala wa Barry Ferguson na akaendelea kuwa mchezaji wa mara kwa mara katika timu ya kwanza kwa salio ya msimu, kwa kucheza mechi 22 kwa jumla. Alitumiwa na meneja wa Blackburn Mark Hughes kama sehemu ya kiungo cha kati ya cha wachezaji tatu katika mfumo wa 4-5-1, hatua ambayo ilipelekea Blackburn kufungwa mabao chache na kuondoka hatarini ya kushukishwa katka ligi ya daraja ya pili.

Hughes baadaye alirejea mfumo wa 4-4-2, ambayo kamwe haikuonyesha ubora wa mchezaji huyu. Mchezo wake ambao haukuvutia kutokana na mfumo huu wa 4-4-2 ikiwa ni pamoja na ukosefu wake wa uwezo dhahiri wa kiufundi, ilipelekea mashabiki wengine wa Blackburn kumfanyia Mokoena maskhara. Kutoka hapo na kuendelea, alijipata adimu akitumiwa kama kiungo wa kati wa kushikilia mpira katika mfumo huo wa 4-5-1 na alikuwa anacheza kama mbadala wa nusu ya pili, aliyetumika kulinda uongozi katika mechi ambazo Blackburn ilikuwa inaelekea kushinda. Huku Robbie Savage akiwa kwa sababau ya jeraha, Mokoena alianza mechi mingi za Rovers mwaka wa 2007 na alifunga bao lake la kwanza kwa Blackburn Rovers katika raundi 6 ya Kombe la FA katika ushindi dhidi ya Manchester City tarehe 11 Machi 2007. Hata hivyo, alionyeshwa kadi nyekundu katika mechi hiyo baada ya kupata kadi mbili za njano. Alifunga bao lake la pili na la mwisho la Blackburn dhidi ya Sunderland mnamo Februari 2009, tena katika kombe la FA. Mokoena alicheza mechi yake ya mwisho kwa Blackburn Rovers mnamo 24 Mei 2009. Siku hiyo hiyo alitangaza kuwa alikuwa anajiunga na Portsmouth kwa mkataba wa miaka mitatu.

Kimataifa hariri

"Mbazo" au "The Axe", jina lake maarufu kutokana na makabiliano yake ya nguvu kama ilivyoonekana wakati alimkabili mchezaji mwenzake wa timu ya Bafana Bafana, Steven Pienaar, katika mechi kati ya Everton na Portsmouth, ni mchezaji mwenye umri mdogo zaidi milele ambaye ameiwakilisha Afrika Kusini [9] baada ya kucheza mwaka 1999 katika mechi za kufuzu kushiriki katika Michezo ya Olimpiki ya mwaka wa 2000, na kuendelea kuichukua nafasi ya Lucas Radebe kama nahodha wa nchi yake.

Mnamo Januari 2008, Mokoena alikuwa nahodha wa upande wake wa Afrika Kusini katika Kombe la Mataifa ya Afrika ambao ulifanyika nchini Ghana, na kutokana na fomu yake ya kuvutia katika mechi zote tatu ambazo alishiriki, iliripotiwa kuwa alikuwa shabaha kwa pande kadhaa za Ulaya, kama vile Manchester City, klabu yake ya zamani Ajax na Schalke 04. Mnamo 16 Machi 2009, Mokoena alitangaza kuwa hatakuwa akisaini mkataba mpya na Blackburn, ambayo ilikuwa inaisha mwishoni mwa msimu kutokana na ukosefu wake wa kucheza.

Mabao ya kimataifa hariri

# Tarehe Ukumbi Mpinzani Mabao Tokeo Mashindano
[1] 8 Oktoba 2006 Lusaka,Zambia Zambia 1-0 1-0 mechi ya kufuzu kushiriki mchuano wa Kombe la Mataifa ya Afrika

Marejeo hariri

Viungo vya nje hariri